Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
SHIRIKA la Viwango Tanzania(TBS)limeshiriki katika Maonesho ya wiki ya maziwa yanayofanyika katika Viwanja vya Sheikh Abeid Karume lengo ikiwa ni kuelimisha wajasiriamali na wadau katika sekta ya maziwa kuhusu namna ya kuthibitisha ubora wa bidhaa ya maziwa na bidhaa nyinginezo zinazotokana na maziwa.
Maofisa wa TBS wametumia nafasi hiyo kutoa mwito kea wajasiriamali kuthibitisha bidhaa hizo kwani ni bure na kutoa mwito pia kwa wananchi kununua bidhaa zilizothibitishwa na TBS.
"TBS)tumeshiriki katika Maonesho ya wiki ya maziwa ambayo yanayofanyika Viwanja vya Sheikh Abeid Karume,lengo letu kubwa hapa ni kuelimisha wajasiriamali na wadau katika sekta ya maziwa katika kuthibitisha ubora wa bidhaa ya maziwa na bidhaa nyinginezo zinazotokana na maziwa,'amesema mmoja wa maofisa wa TBS wakati wa maonesho hayo.
Ofisa Udhibiti Ubora kutoka TBS Stanford Matee akitoa elimu kwa baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Arusha juu ya masuala ya udhibiti ubora pindi walipotembelea banda letu katika maonesho ya wiki ya maziwa yanayofanyika jijini Arusha
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...