Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza na Kikosi kazi kinachofanya Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai jijini Dodoma.
Baadhi ya washiriki wa kikosi kazi kinachofanya maboresho ya mfumo wa haki jinai .
Mkurugenzi Msaidizi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki Wizara ya Katib na Sheria Bw. Patience Ntwina akitoa maelezo mafupi kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani Ndg. Ramadhani Kailima kuhusu kazi ya Maboresho ya mfumo wa haki jinai inayofanywa na kikosi kazi maalum jijini Dodoma ambapo Ndg. Kailima aliwatembelea na kuzungumza nao.


Naibu Katibu Mkuuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Ndg. Ramadhani Kailima awataka wadau wa Maboresho ya mfumo wa Haki Jinai kuibua changamoto zinazokwamisha ufikiwaji wa Haki Jinai. 

Hayo ameyasema alipotembelea kikosi kazi kinachopitia Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai na kuwataka wataalam kuupitia mfumo huo kwa umakini na kufuta viashiria vyote vya ukiukwaji wa Haki Jinai nchini ikiwemo tabia ya baadhi ya viongozi kuweka watu ndani bila kufuata utaratibu wa kisheria. 

“Mnapoendelea na maboresho ya Haki Jinai mhakikishe mnatafuta namna ya kufuta ukiukwaji wa Haki jinai” amesema .Naibu Katibu Mkuu huyo amewataka wadau wa mkutano huo kuweka wazi mambo yote yenye Ushahidi wa uvunjwaji wa haki Jinai ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa ukiukwaji wa Haki Jinai. 

Akitolea mfano namna wananchi wanavyovunjiwa haki zao na polisi kwa kuwekwa ndani bila kufuata sheria hasa wanapoamria na viongozi, Kailima alisema kabla ya kumweka mtuhumiwa ndani polisi wajiridhishe kwa kufanya upelelezi juu ya tuhuma husika ndipo wamweke mtuhumiwa ndani hapo ndipo haki jinai itakuwa imetekelezwa. 

Aidha, amewataka wadau kufanya kazi ya maboresho hayo kwa bidii na wasichoke kwani maboresho hayo yatasaidia wananchi kupata haki zao. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...