Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya Wizara yake. Kikao hicho kilifanyika Ukumbi wa Wizara jijini Dodoma, leo. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akimpa hati ya kiapo Afisa Utumishi wa Wizara hiyo, Andrew Kiangi, kuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza na Uhamiaji inayoshughulikia masuala ya Utumishi na Utendaji wa Askari wa Majeshi hayo. Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo jijini Dodoma leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto meza kuu) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, wakiongoza kikao cha Wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza katika kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya Wizara. Kikao hicho kilifanyika Ukumbi wa Wizara, jijini Dodoma, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akimuapisha Afisa Utumishi wa Wizara hiyo, Andrew Kiangi, kuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza na Uhamiaji inayoshughulikia masuala ya Utumishi na Utendaji wa Askari wa Majeshi hayo, katika Ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dodoma, leo. Kulia (aliyekaa) ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...