MSANII marufu nchini Tanzania katika muziki wa kizazi kipya a.k.a Bongo Fleva ambaye kwa sasa yuko kwenye ubora wake Rajab Abdull Kahali a.k.a Harmonize amemuandikia ujumbe mzito Rais Dk.John Magufuli.
Katika ujumbe huo Harmonize ameandika hivi ; kipaji na umaarufu ni tunu ambayo Mungu humpatia amtakaye kwasababu maalum!!!
Kwa lugha nyingine , ni sauti yenye mamlaka ya peke ambayo hupendwa na kushabikiwa na wengi yaani watoto, kwa watu wazima, wanawake kwa wanaume. Hakuna awezaye kujipa umaarufu au kujipa bila matakwa yake Mungu Baba...!!!
Nitakuwa mpumbavu sana endapo nitaliona jambo baya na kupitia sauti hii au tunu hii ambayo Mungu kanijaalia nikalifumbia macho tena hata M/Mungu anaweza Kanijalia Nikalifumbia Macho Tena Hata M/Mungu Anaweninyang'anya maana hatokuwa na faida tena!!!!
Lakini nitakuwa mpumbavu zaidi nikiliona jambo jema hasa linalogusa watu waliosababisha mimi leo hii naitwa Harmonize eti nilifumbie macho kwa kuingiwa na hofu ya aina yoyote ile...!!!!
Kiukweli nitakuwa sijaitende haki ile sauti yenye mamlaka na ushawishi niliyo tunukiwa tena sio kwa unjanja wangu...!!!!
Naomba niseme kwa heshima na taadhima nikiwa kama Mtanzania Mzalendo niliyezaliwa Mtwara naipongeza Saaaana Serikali ya Awamu ya Tano (5).
Pia nichukue fursa hii kuzishukuru Serikali za Awamu zote....!!!! Tukufu zilizopita kwa misingi mizuri ambayo tunajivunia sisi na vizazi vijavyo...!!
Tamanio langu ujumbe huu utakufikia na kukuongezea nguvu ya kutujali zaidi wanyonge na kupambana kwa niaba ya Taifa letu tukufu....!!!!!
Kwako Mhe.John Pombe Magufuli #TanzaniaKwanza #JESHI #KONDEGANG4EVERYBODY #WCB4LIFE
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...