KINA mama wameshauriwa kuwanyonyesha watoto wao kuanzia umri 0 hadi miezi sita ili waweze kupata afya bora ambayo itamsaidia kumjenga kimwili na kiakili katika ukuaji wake.

Hayo yalisemwa na Mratibu Lishe Mkoa wa Dar es Salaam, Neema Kweba ambapo alisema kuwa kitendo cha kuacha kuwanyonyesha kabla ya muda kwa kisingizio cha maziwa hayatoki kunaweza kusababisha udumavu wa mwili na akili.

Alisema mtoto anatakiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama kuanzia anapozaliwa (umri 0) hadi umri wa hadi umri wa miaka miwili na zaidi huku akifikisha miezi sita anatakiwa kupewa vyakula mchanganyiko yakiwamo maziwa ya mama yake.

Alisema maziwa ya mama yana virutubisho vingi ambavyo vinasaidia katika ukuaji wake jambo ambalo linawamfanya mtoto kuwa na afya bora Na kuendelea kukua bila ya matatizo yoyote.

"Kuna baadhi ya kina mama wana tabia ya kuwaachisha watoto kunyonya kabla ya wakati kwa kisingizio cha maziwa hayatoki, jambo ambalo ni uongo na kwamba linaweza kusababisha udumavu kwa mtoto kwa kushindwa kukua ipasavyo," alisema Kweba.

Aliongeza kuwa, hivyo basi wanapaswa kubadilika na kunyonyesha watoto wao kuanzia umri 0 hadi miaka miwili na kwamba wakifikisha umri wa miezi sita wanapaswa kuwaanzishia vyakula mchanganyiko vyenye virutubisho huku akiendelea kunyonya,hali ambayo itaimarisha afya yake.

"Ninawasihi wanawake wenzangu acheni tabia ya kusingizia maziwa hayatoki ili muweze kuwaachisha watoto wenu kabla ya wakati, kufanya hivyo kunaweza kusababisha udumavu kwa mtoto au kukosa afya bora, kwa sababu maziwa ya mama ni muhimu kwa afya yake na kwamba yanamsaidia katika ukuaji wa afya ya mwili na akili," alisema Kweba.

Aliongeza kuwa, mtoto anapokosa afya bora, madhara yake ni makubwa ikiwa ni pamoja na kupata udumavu au utapiamlo, ukosefu wa kinga za mwili ,jambo ambalo linaweza kusababisha ubongo wake kushindwa kukua ipasavyo.

Alisema kuwa kila mzazi anayenyonyesha ana wajibu wa kuhakikisha anamnyonyesha mtoto hadi afikie umri wa miaka miwili au zaidi huku akiendelea kumpa chakula mchanganyiko, jambo ambalo litamsaidia mtoto kuwa na afya bora pamoja na kumkinga na maradhi.

Alisema mkakati wa Mkoa ni kuhakikisha kuwa wanaendelea kutoa elimu ya lishe kwenye vituo vya afya, zahanati na hospitali pamoja na majumbani ili kuwaelimisha wazazi au ndugu wanaobaki na watoto ili waweze kuzingatia elimu ya lishe bora kwa mtoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...