![]() |
Mlango wa kuingilia ndani ya Stendi kuu ya mabasi ya Tabora mjini. |
Muonekano wa Stendi kuu ya mabasi ya Tabora mjini.
![]() |
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Joseph Kashushula akizungumza kuhusiana na halmashauri hiyo kubuni chanzo kipya cha mapato |
Na Editha Edward, Michuzi TV Tabora
Halmashauri ya manispaa ya Tabora mjini imepata chanzo kipya cha mapato ya ndani kupitia Stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani na wilayani ambapo kila mtu anayeingia ndani ya Stendi hiyo atatozwa kiasi cha shilingi 200 ili kupata huduma ya kusafiri.
Akizungumza ofisini kwake kaimu Mkurugenzi wa halmashauri Tabora manispaa Joseph Kashushula (pichani) amesema chanzo hicho kimebuniwa hivi karibuni ambapo pesa ambayo itapatikana hapo itaweza kusaidia huduma ambazo ni bora kwa wananchi wa manispaa hiyo zikiwemo za kiuchumi kiafya na kielimu
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara ndani ya Stendi hiyo Juma Iddy na Fadhili Hussein wamesema utaratibu waliouweka halmashauri ni mzuri kwani unaongeza mapato ya ndani na uchumi kwa ujumla ila unachangamoto za kjuimarisha miundombinu ya stendi.
Aidha hivi karibuni kwa mujibu wa kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Tabora Joseph Kashushula amesema halmashauri itakuwa inakusanya zaidi ya shilingi Milioni 408 kwa mwezi huku ikiendelea na mikakati ya kubuni vyanzo vingine vya mapato ya ndani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...