MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu mnamo Novemba 7, mwaka huu inatarajia kutoa hukumu dhidi ya kesi ya ya inayomkabili aliyekuwa  Rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wenzake watatu.

Mbali na Malinzi,  washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu  Mtendaji wa zamani wa Shirikisho hilo, Celestine Mwesigwa,aliyekuwa mhasibu  Nsiande Mwanga na Karani Flora Rauya.

Mapema leo Oktoba 25, Wakili wa Serikali Ester Martin alidai Mahakani hapo kuwa kesi hiyo ambayo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Maira Kasonde imekuja kwa ajili ya kupangiwa tarehe ya hukumu lakini hakimu Kasonde amepata udhuru wa kikazi hivyo Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi amesema hukumu dhidi ya washtakiwa hao itasomwa Novemba 7, mwaka huu.

Hukumu hiyo imepangwa kutolewa baada ya washtakiwa hao kumaliza kutoa utetezi wao ambapo walijitetea wenyewe huku upande wa mashtaka ulikuwa na jumla ya mashahidi 15 pamoja na vielelezo 9.

Julai 23 mwaka huu washtakiwa hao walikutwa na kesi ya kujibu aada ya mashahidi wa upande wa mashtaka kumaliza kutoa ushahidi.

Katika kesi  hiyo, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 20 yakiwamo ya kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha wa dola za Marekani  173,335.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...