Ndege Inatua Leo Katika Ardhi ya Tanzania  ni Ndege ya 8 KWENYE Orodha ya Ndege za AIR TANZANIA 

1. Boeing 787-8 Zipo 2
2. Forker 50 Ipo 1 
3. Bombardier Dash 8-400 Zipo 3
4. Bombardier Dash 8-300 Ipo 1 
5. Airbus  A220-300 Zipo 2 


Ndege Hii Mpya Imesajiliwa Kwa Usajili Namba 5H-TCJ na Imepewa Brand Name ya Visiwa vya RUBONDO ISLAND Vilivyopo  Mkoani Mwanza Vyenye Ukubwa wa Kilometre za Mraba 456.8 Sawa na Kushabihiana Ukubwa wa Manispaa ya KINONDONI Mkoa wa DAR ES SALAAM

Ndege Mpya ya Air TANZANIA Boeing 787-8 Ina Uwezo  wa Kutembea Kilometres 13620 Sawa na saa zaidi ya 12 Hewani Bila ya Kusimama 

Inabeba Lita 101,000 za Mafuta na Ina Ukubwa wa MITAA 56.72 Yaani Ni Sawa na Nusu ya Uwanja wa Mpira wa Miguu

Inabeba Jumla ya Abiria 262 

Ina Uwezo wa Kubeba Uzito wa Tani 227 Yaani 227,930Kg Wakati wa Kupaa Uzito wa Hujumuisha Uzito wa Chombo,Mizigo,Mafuta na Inapotua Inatakiwa Iwe na Tani  172 za Uzito, Hii Inatokana na Kupungua Kwa Kiasi Cha Mafuta Wakati wa Kutua .

Sifa ya Ndege Hii Ina Uwezo Mkubwa wa Kuhimili Hali Nzito ya Hewa Ikiwa KWENYE Umbali Mrefu Kwenda Juu 

Leo Tunaipokea Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JNIA 



Mgeni RASMI ni Mhe RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, H:E Dr JOHN POMBE MAGUFULI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...