Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike akikagua Paredi Maalum lililoandaliwa na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza lililofanyika Oktoba 25, 2019 katika Viwanja vya Chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike akiwa katika jukwaa akipokea salaam ya heshima kutoka kwa Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza(hawapo pichani).
Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza wakipita mbele ya Mgeni rasmi katika Sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika Viwanja vya Chuo cha Jeshi la Magereza, KPF Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP Phaustine Kasike(kushoto) akimvisha cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza mmoja wa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza ambaye amefanya vizuri zaidi katika Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa muda wa miezi minne.
Baadhi ya Maofisa wa Kike wa Jeshi la Magereza ambao ni miongoni mwa wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza wakiwa tayari wamevishwa vyeo vipya kama wanavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP Phaustine Kasike akitoa hotuba fupi kwa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza(hawapo pichani).
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi kama wanavyoonekana katika picha.
Mhitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza akisoma risala mbele ya mgeni rasmi.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP – Phaustine Kasike(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa Wahitimu wa Mafunzo ya Maafisa Wakaguzi Wasaidizi wa Magereza waliosimama mstari wa nyuma(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...