Real Madrid iko tayari kuipatia Manchester United £90m pamoja na mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 30, ili kumsajili Paul Pogba, lakini inataka mchezaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 26 kuimarisha kiwango chake cha mchezo uwanjani . (El Desmarque, in Spanish)
Real Madrid ina mpango wa kumuuza mshambuliaji Bale na kiungo wa Colombia James Rodriguez 28 ili kupata fedha za kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa na PSG Kylina Mbappe 20. (Calciomercato)
Wakati huohuo, rais wa Real Madrid Florentino Perez ana mpango wa kufanya kila kitu katika uwezo wake ili kumnyakua Mbappe katika uwanja wa Bernabeau msimu ujao. (AS)
Bayern Munich inafikiria uhamisho wa mwezi Januari wa beki wa Atletico Bilbao na Uhispania Unai Nunez na wamefanya mazungumzo na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 ambaye pia anahusishwa na uhamisho wa kuelekea Arsenal na Everton. (Goal.com)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...