Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa ccm (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kiongosi akiwana baadhi ya viongozi wa UVCCM mkoa wa Iringa pamoja na wadau wa chama cha mapinduzi Mkoa wa iringa 


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MWENYEKITI wa umoja wa vijana wa ccm (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kiongosi amewataka wanasiasa mbalimbali wanaousaka ubunge wa jimbo la Iringa Mjini kufuata misingi ya chama ili wapite kwenye kanuni na taratibu za chama.

Akizungumza na viongozi wa UVCCM mkoa wa Iringa Kihongosi alisema kuwa viongozi wote wanaoutafuta ubunge katika jimbo la Iringa mjini wanatakiwa kufuata utaratibu unatakiwa na chama cha mapinduzi ili kumpata kiongozi bora.

“Katika kipindi cha miaka kumi sasa tumekuwa tukipoteza jimbolaIringa mjini kwa kuwa na makundi kutokana na viongozi warafi na waroho wa madaraka kwakutoa rushwa kwa wapiga kura ili waweze kupata ubunge,kwa sasa hatuwezi kukubali swala hilo kwa kuwa tunahujumiwa kutokana na makundi ambayo yamekuwa yakitokeza kipindi cha uchaguzi” alisema Kihongosi

Kihongosi alisema kuwa kumekuwa na viongozi wanaoutaka ubunge Iringa Mjini wameanza kufanya kazi wanavyojitakia wao bilakufuata njia sahihi ambazo zinatakiwa,badala yake wamekuwawakitoa fedha kwa baadhi ya wadau kwa lengo la kutengeneza makundi ambayo hayana faida kwa wananchi wa Manispaa ya Iringa.

Aidha Kihongosi aliwataka vijana wa chama cha mapinduzi kukataa mara moja kutumika kuwa daraja kuwatafutia ubunge viongozi ambao hawana msaada katika jumuiya katika kuleta maendeleo kwa vijana ambao ndio wamekuwa wakitumia kuleta ushindi kwamgombea wa chama cha mapinduzi.

“Vijana acheni mara moja kutumika kwa viongozi wasaka tonge ambao wamekuwa wakipata madaraka hawakumbuki mchango wa vijana wakati wa kukitafuta cheo chake”alisema Kihongosi

Kihongosi alisema mwaka 2015 kulikuwa namakundi makubwa mawili ambayo yalikuwa katika ya wenyeviti na makatibu na kupelekea kupoteza jimbo la Iringa Mjini na kulikuwa na mvurugano mkubwa kweli ambao ulimpa tena ubunge Mchungaji Petter Msigwa.

“Nitasikitika sana kuona kijana mmoja ambaye ni kiongozi kumbeba mgombea furani,nikikutambua mapema nitakupeleka kwenye kamati husika na tutakuondoa kwenye nafasi ambayo uponayo hivi sasa ili usituvuruge kwenye harakati zetu za kulikomboa jimbo la Iringa Mjini” alisema Kihongosi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...