Viongozi waandamizi wa muugano wa Tanzania Election Alliance (TanEA ) pichani, kulia Mwenyekiti wa Muungano huo Michael Kyande,Katibu wa Taasisi ya The Right Way (TRW),Gideon Mazara,Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Action for Change (ACHA),Bi.Martina Kabisama pamoja na Mwenyekiti wa ACHA Justina Shauri wakionesha vijarida vya elimu ya Uraia na Uchaguzi  vitakavyosambazwa kwa Wananchi baada ya kuzindua Muungano wao leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam.Picha na Michuzi JR (MMG).
 Viongozi waandamizi wa muugano wa Tanzania Election Alliance (TanEA ) pichani  wakishuhudia Mwenyekiti wa Muungano huo Michael Kyande (kulia), akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa Muungano huo leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi  Mtendaji wa Taasisi ya Action for Change (ACHA),Bi.Martina Kabisama akizungumza leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam
 wakati wa uzinduzi wa Muungano wa Tanzania Election Alliance (TanEA ) wenye lengo la kutoa elimu ya Uraia na Uchaguzi kwa Wananchi kwa kuanza na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Action for Change (ACHA) Justina Shauri akifafanua jambo katika uzinduzi huo leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam
Mratibu wa muugano wa Tanzania Election Alliance (TanEA ) ,Rhoda Kamungu akiwakaribisha wageni waalikwa pamoja na mgeni rasmi wakati wa uzinduzi huo,uliofanyika leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam


 Viongozi waandamizi wa Tanzania Election Alliance (TanEA ) wakifuatilia jambo wakati wa uzinduzi huo leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam

Na Said Mwishehe,Michuzi Globu ya jamii
TAASISI ya Action For Change(ACHA)  na Right Way  (TRW)  waungana kwa pamoja na kuzindua muungano wao unaofahamika kwa jina la Tanzania Election Alliance kwa lengo la kushirikiana kwa pamoja kutoa elimu ya uraia na kueleza kuwa katika kutekeleza majukumu yao watashirikiana kwa karibu na wadau mbalimbali wanaohusika na chaguzi ukiwemo uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi mkuu mwaka 2020.
Muungano huo umezinduliwa leo Novemba 1, mwaka 2019 jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine viongozi wake wameeleza kuwa malengo yao, matarajio yao na ushiriki wao katika kujadili mafanikio na changamoto zilizopo katika michakato  mbalilmbali ya  uchaguzi.
Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa ACHA Martina  Kabisama amesema wameona iko haja ya wao kuunganisha nguvu ya pamoja na kufanya kazi  zinazohusiana na uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2019 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
"Naomba nieleweke vizuri vibali ambavyo tumevipata ni kwa ajili ya kutoa elimu ya uraia pamoja na ile ya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu mwaka 2020,"amesema  Kabisama na kuongeza muungano huo upo kihalali kwani umefuata tararibu zote na hata asasi zilizounda muugano huo zimesajiliwa na zinatambuliwa kisheria.
Amefafanua zaidi wameamua kuwa na muungano huo baada ya kuona ndani yao wamo wabobezi wa masuala ya uchaguzi ambapo waliangalia kabla ya kufikia uamuzi huo waliangalia masuala ya uchaguzi na ushiriki wa wananchi na kubaini wanayo nafasi ya wao kuunganisha nguvu ili chaguzi ziwe na mafanikio kabla na baada ya chaguzi.
"Katika kufuatilia tulibaini kuna mafanikio makubwa katika chaguzi zetu na wakati huo huo kuna changamoto, hivyo tumeona tuje na huu muunganiko kwa ajili ya uchaguzi kwani hakuna sababu ya sisi kubaki nyuma lazima tushiriki ili tuwe sehemu ya kuondoa changamoto zilizopo.
"Katika changamoto hizo zinaweza kuwa zinazohusu wananchi, sheria au vyombo vinavyosimamia uchaguzi aidha wa  Serikali za Mitaa au Uchaguzi Mkuu .Hivyo lazima tukae na kutafuta ufumbuzi kwa pamoja,"amesema.
 Hata hivyo amesema katika kuhakikisha muungano huo unakwenda vizuri waliamua kujiwekea malengo yao kwani kuungana bila kuwa a malengo ni rahisi kuvunjika. Ametumia nafasi hiyo kueleza taasisi za chaguzi zipo na zinapita  katika michakato mbalimbali hadi inapofikia hatua ya kupiga kura na kisha kuingia katika mchakato wa kuanza uchaguzi mwingine.
"Uchaguzi ni kama duara, tunapomaliza uchaguzi mmoja tunaanza safari ya uchaguzi mwingine.Hivyo muungano wetu nao tutashiriki kikamilifu Uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na baada ya hapo tutaendelea na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020,"amesema .
Ameongeza  taasisi ambazo zinahusika na chaguzi za Serikali za Mitaa ni Wizara ya Nchi ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) , hivyo ameahidi kushirikina na TAMISEMI kuhakikisha uchaguzi huo wa mitaa unakwenda vizuri  na katika uchaguzi mkuu mwaka 2020 watashirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC).
Wakati huo huo Kabisama amezungumzia umuhimu wa Watanzania kushiriki katika chaguzi huku wakihakikisha nchi inaendelea kuwa na amani na usalama na kuongeza wajibu wa kila Mtanzania mwenye sifa ya kupiga kura kujiandikisha na siku ya kupiga kura anakwenda kuchagua kiongozi au viongozi kwa maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa ACHA Justina Shauri amesema vyombo vya habari vinadhamana kubwa ya kufikisha taarifa na hivyo wanategemewa sana katika kufikisha habari zinazohusu elimu kwa mpiga kura na mchakato wa kupiga kura.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Shauri amesisitiza umuhimu wa uhuru wa demokrasia kwa kuhakikisha watu wanaachwa wafanya kazi za uchaguzi kwa mujibu wa sheria na kama watu wanataka kuundamana basi taratibu zifuatwe.
Pia Shauri amezungumzia suala la uangalizi wa ambapo katika hilo amesema waangalizi wa uchaguzi wanapaswa kutekeleza majukumu yao na hiyo itasaidia kutambua changamoto zilizopo na hatimaye zitapatiwa ufumbuzi.

"Ukiwa makini katika suala la uangalizi wa uchaguzi kuna mambo tu utayabaini aidha ya mafanikio au changamoto.Hivyo itakuwa rahisi kuboresha chaguzi zetu maana yale ambayo yatakuwa kama sababu za kukwamisha mchakato yatapata ufumbuzi,"amesema Shauri na kuongeza hivyo moja ya majukumu yao ni kutoa elimu pia kwa waangalizi nini wafanye ili kazi hiyo kufanyika kwa ufasaha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...