Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya wilaya ya Hai,Juma Massatu amesema wanachama 110 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliojitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi ya Wenyeviti wa Mitaa, vijiji na vitongoji wamepita bila kupingwa.
Idadi hiyo ni Kati ya vitongoji 294 ambavyo wanachama wa vyama mbalimbali walijitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi hizo ambapo hawakuweza kuchukua na kurejesha fomu hizo.
Tayari Msimamizi huyo was uchaguzi amewatangaza rasmi wagombea hao kuwa ndio washindi katika vitongoji hivyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...