Afisa Elimu Msingi  wa Wilaya ya Tandahimba Khadija Mwinuka amesema kuwa wakazi katika vijiji  Wilayani  humo wameanza  kuchimba matundu vyoo kutekeleza Kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara

Mwinuka amesema wananchi wamekubaliana kuchimba matundu ya vyoo 50 kwa shule za msingi Ruvuma na Mihambwe 

Katika Kijiji Cha Chitoholi na Mkupete tayari nao wameanza ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule ya msingi Chitoholi na Mkupete

"Tupo pamoja  katika Kampeni ya shule ni choo ambapo wananchi  wamekubaliana kujenga matundu ya vyoo katika shule zao za msingi kwa kujitolea kwa Hali na Mali ili tatizo Hilo lisiwepo katika maeneo yao,"alisema Mwinuka

Kampeni ya shule ni choo ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa  la  kuondoa tatizo la uhaba wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari ndani ya Mkoa wa Mtwara
 Ujenzi wa Matundu ya vyoo ukiendelea
 Wanakijiji wakijitolea katika maandalizi ya kujenga matundu ya vyoo 

 Wanakijiji wakijitolea katika maandalizi ya kujenga matundu ya vyoo
Wananchi wakijadiliana ili kufikia malengo yao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...