Na Zainab  Nyamka, Globu ya Jamii

Uongozi wa Klabu ya Yanga umemsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi Kaimu Meneja wa timu hiyo Dismas Tena baada ya kuwavalisha sare zisizo halali benchi la ufundi na wachezaji.

Taarifa hiyo imetolewa na Idara ya habari na Mawasiliano Yanga leo.

Katika taarifa hiyo, inadaiwa Dismas aliwavalisha sare benchi la ufundi na wachezaji ambazo hazijatengenezwa na mdhamini wa Klabu hiyo GSM kwa mujibu wa mkataba.

Aidha, wamesema uongozi umeamua kumsimamisha kwenye majukumu yakr ya umeneja ili kupisha uchunguzi wa kina wa suala hilo na hatua zaidi za kinidhamu zitachukuliwa kwa kila aliyehusika.

Uongozi wa Yanga umewaomba mashabiki na wanachama waendelee kununua bidhaa halali zinazotengenezwa na kusambazwa na mdhamini wao GSM ili kuhakikisha Yanga inaendelea kunufaika na nembo yake pamoja na matumizi ya nembo hiyo.

Pia, wanaomba radhi kwa mdhamini wao kwa kitendo kilichofanywa na Meneja wao na kuhakikisha hakitajirudia tena na wamewatahadharisha wote wanaotengeneza, kusambaza na kuuza bidhaa zenye nembo ya Yanga waache mara moja ili kuepuka kuchukuliwa hatua za Kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...