BODI ya Taifa ya Wahasibu  na Wakaguzi  wa Hesabu nchini NBAA,  imepitisha na kutangaza matokeo ya watahiniwa 6179  waliofanya mtihani kati ya Oktoba 29  hadi Novemba, 2019 katika ngazi mbalimbali za masomo.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) CPA Pius  Maneno imebainisha kuwa matokeo hayo yanafuatia mitihani iliyofanyika katika vituo 11 vya mitihani kutoka mikoa kadhaa ya Tanzania Bara na Visiwani.

Alisema mitihani hiyo ilihusisha watahiniwa katika hatua ya kwanza na ya Pili katika ngazi ya cheti cha utunzaji wa  Hesabu (ATEC I , ATEC II) zenye masomo manne kila moja na ngazi ya taaluma, Hatua ya Awali/Msingi (Foundation Level) yenye masomo matano, Hatua ya Kati (intermiediate Level), yenye masomo sita na hatua ya mwisho yenye masomo manne.

"Watahiniwa  waliosajiliwa  walikuwa  6,805 kati ya hao watahiniwa   626 sawa na asilimia  9.2 hawakuweza  kufanya  mitihani  hiyo kwa sababu mbalimbali. Hivyo  watahiniwa   waliofanya   mitihani   walikuwa   6,179  sawa  na  asilimia
90.8.  Kati ya watahiniwa   waliofanya  mitihani  hiyo  watahiniwa   237 ambao ni asilimia 3.8 wamefaulu  mitihani  katika mkao mmoja, wengine  41 sawa na asilimia  0.7 wamefaulu  kwa  kufaulu  masomo  walioyokuwa   wameshindwa katika  mitihani  ya nyuma,  wengine  921  sawa  na  asilimia  14.9  wamefaulu mitihani  yao kwa  kufaulu  masomo  waliyokuwa   wamebakiza," alisema Maneno.   

Pia alisema  watahiniwa     1,199    sawa   na   asilimia    19.4   wamefaulu    mitihani    yao na kwamba watahiniwa   wengine   2,678  sawa  na  asilimia   43.3  wamefaulu   baadhi  ya masomo  katika  ngazi  mbalimbali  na watahiniwa  2,302  waliobakia   sawa na asilimia  37.3 hawakufaulu  mitibani  yao.

Awali, taarifa hiyo ilieleza kuwa watahiniwa waliosajiliwa    walikuwa   765  kati  ya  hao watahiniwa   77 sawa na asilimia  10.1 hawakuweza   kufanya  mitihani hiyo kwa  sababu  mbalimbali na hivyo kufanya ndani ya watahiniwa   waliofanya  mitihani kuwa  688   sawa  na  asilimia   89.9.     

Pia imeelezwa kuwa kati   ya  watahiniwa  688 waliofanya  mitihani katika ngazi hii watahiniwa  135 ambao ni asilimia
19.6 wamefaulu   mitihani  katika  mkao  mmoja huku wengine  04  sawa  na asilimia   0.6  wamefaulu   masomo  waliyokuwa   wameshindwa  katika mitihani  ya nyuma,  wengine   168 sawa  na  asilimia  24.4  wamefaulu mitihani   yao  kwa  kufaulu   masomo   waliyokuwa   wamebakiza.   

Imeelezwa kwa ujumla watahiniwa  307 sawa na asilimia 44.6 wamefaulu  mitihani  yao na watahiniwa  255 sawa na asilimia  31.7 wamefaulu  baadhi  ya masomo katika  ngazi  hii.  Watahiniwa   126  waliobakia   sawa  na  asilimia   18.3 hawakufaulu  mitihani  yao.

Aidha, katika hatua ya  Kati, waliojisaliwa walikuwa   3,685   kati  ya  hao watahiniwa  375 sawa na asilimia 10.2 hawakuweza   kufanya  mitihani kutokana na sababu  mbalimbali. watahiniwa  waliofanya  mitihani walikuwa 3,310 sawa na asilimia 89.8.   Kati ya watahiniwa  3,310 waliofanya  mitihani  katika ngazi hii  watahiniwa   33 ambao ni asilimia
1.0  wamefaulu   mitihani   katika  mkao  mmoja,   wengine  31  sawa  na asilimia     0.9     wamefaulu     kwa     kufaulu     masomo waliyokuwa wameshindwa    katika   mitihani  ya  nyuma.

Alisisitiza kuwa asilimia    12.4   wamefaulu     mitihani yao kwa kufaulu    masomo waliyokuwa    wamebakiza, hivyo  Kwa   ujumla   watahiniwa    474   sawa   na asilimia   14.3  wamefaulu   mitihani   yao.  Watahiniwa   1,529  sawa  na asilimia    46.2   wamefaulu baadhi  ya masomo    katika    ngazi   hii. Watahiniwa    1,307  waliobakia   sawa  na  asilimia   39.5  hawakufaulu mitihani  yao.

Katika hatua ya mwisho, watahiniwa    337   sawa   na asilimia   15.7  wamefaulu   mitihani   yao.  Watahiniwa    784  sawa  na asilimia    40.8   wamefaulu    baadhi    ya   masomo    katika   ngazi   hii. Watahiniwa    802   waliobakia    sawa   na   asilimia   41.7   hawakufaulu mitihani  yao.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo ametoa pongezi kwa wale wote waliofuzu mitihani yao na kuwataka wale ambao hawajafuzu kutokata taama badala yake waongeze bidii zaidi katika masomo yao ili wawezo kufuzu mitihani ijayo.

Alisema mitihani  ya katikati  ya muhula  kwa  ajili ya masomo  ya A5 Business Law,  B5  Performance   Management,   C3  Corporate Finance and  C4Advanced    Taxation itafanyika  Februari 25 na 26  2020 katika  kituo  cha Dar es Salaam hivyo,   wanaopenda  kujisajili katika mitihani hiyo wanakaribishwa.

"Mahafali   ya  42  ya  NBAA   yatafanyika   Oktoba 3,  2020. Tangazo   rasmi  kuhusu  mahafali   hayo  litawekwa   kwenye   tovuti  ya bodi. Wale  wote waliofaulu  mitihani  ya ATEC  II na  CPA (T) pamoja  na wale wa CPA (T) Equivalent  wanatakiwa  kuwasilisha  picha zao kwa ajili ya kutengenezewa    vyeti  kabla  ya  Januari   30, 2020.  Tangazo  juu  ya namna  ya kuwasilisha  picha hizo liko kwenye tovuti ya Bodi," alisema.

BOFYA HAPA KUYATAZAMA MATOKEO HAYO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...