Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amewasilisha tamko linalohusu Mapato,Rasilimali na Madeni ya viongozi katika Ofisi ya sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma ikiwa ni utekelezaji wa matakwa ya kisheria na kikatiba.

Tamko hilo limewasilishwa katika ofisi hizo kanda maalumu ya Dar es salaam na katibu wa Rais,  Bwana Ngusa Samike ambaye ametumwa na Mhe Rais akiwa mapumzikoni Chato na limepokelewa na Kamishna wa Sektretarieti ya maadili ya viongozi wa Umma Jaji mstaafu Harold Nsekela.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kupokea tamko hilo Jaji mstaafu Nsekela amesema kitendo alichokifanya Mhe.Rais kimetekeleza takwa la kikatiba Ibara ya 132 (5) (D) linalowataka viongozi kuwasilisha taarifa za tamko la mapato, Rasilimali na madeni mara kwa mara lakini pia ametekeleza sheria no 13 ya mwaka 1995 kingu cha 9.

Jaji mstaafu Nsekela akatumia fursa hiyo kuwakumbusha viongozi wengine kutumia siku 2 zilizobaki kufanya hivyo kabla ya tarehe 31 Desemba katika kutekeleza takwa hilo la kisheria na kikatiba






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...