Meneja wa Bidhaa za Kuwekeza wa Benki ya NBC, Dorothea Mabonye (kushoto), pamoja na Meneja Masoko wa benki hiyo, Alina Maria Kimaryo (wa pili kushoto), wakiagana na mmoja wa washindi wa kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo, Ramdhani Saidi (kulia) muda mfupi kabla ya kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam leo akielekea Seychelles pamoja na mwenza wake. Kupitia kampeni hiyo inayoendelea, washindi wanajishindia safari za kitalii kwenda Seychelles, mbuga za wanyama za Serengeti, bodaboda na pikipiki ya miguu mitatu (Toyo).

 Meneja Masoko wa benki ya NBC,  Alina Maria Kimaryo (kulia), akikabidhi tiketi ya ndege ya kwa moja wa washindi wa kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo, Esther  Ndunguru muda mfupi kabla ya kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam leo akielekea Arusha kufanya utalii katika Mbuga za Wanyama za Serengeti akiwa na mwenza wake. Kupitia kampeni hiyo inayoendelea, washindi wanajishindia safari za kitalii kwenda Seychelles, mbuga za wanyama za Serengeti, bodaboda na pikipiki ya miguu mitatu (Toyo).
 Mshindi wa safari ya kwenda Mbuga za Wanyama za Serengeti wa Ibuka kidedea na NBC Malengo, Esther Ndunguru (kushoto) akikaguliwa tiketi yake kabla ya kupanda ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam leo. Safari hiyo paamoja na mwenza wake inalipiwa na NBC. Washindi wanne wameibuka kidedea na kushinda safari ya kwenda Serengeti pamoja nma wenza wao huku gharama zote zikilipiwa na NBC.  
 Washindi wa kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo wakifungua shampeni muda mfupi kabla ya kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam leo wakielekea Seychelles. Kupitia kampeni hiyo inayoendelea, kila mwezi washindi wanajishindia safari za kitalii kwenda Seychelles, mbuga za wanyama za Serengeti, bodaboda na pikipiki za miguu mitatu (Toyo).
 
 Washindi wa Ibuka Kidedea na NBC Malengo wakitakiwa heri ya safari yao na wawakilishi wa NBC waliowasindikiza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo kabla hawajaondoka.

 Washindi wa Ibuka Kidedea na NBC Malengo wakipozi kwa picha pamoja na  wawakilishi wa NBC waliowasindikiza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo kabla hawajaondoka huku wakiwa wameshika glasi zenye shampeni ikiwa ni ishara ya kuwatakia safari njema.
Washindi wa Ibuka Kidedea na NBC Malengo wakiwa katika hatua ya mwisho ya kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...