Na Karama Kenyunko,Michuzi Globu

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ambapo a wasichana ameendelea kung'ara katika matokeo ya kidato cha nne na darasa la nne huku wavulana wakiongoza kwenye mitihani ya kidato cha pili iliyofanyika Novemba 2019.

Katika matokeo yaliyotangazwa Leo Januari 9,2020 jijini Dar es Salaam, na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza hilo, Charles Msonde amesema kati ya watahiniwa 10  bora tisa ni kutoka Shule ya Wasichana ya ST.Francis ya Mkoani Mbeya huku wengine wakitoka shule za Nyegezi na Sengerema Seminari za mkoani  Mwanza, Feza Boy's (Dar es Salaam) na Shule ya Wasichana  ya Huruma (Dodoma).

Dk Msonde amesema jumla ya watahiniwa wa shule 340,914 sawa na asilimia 80.65 ya watahiniwa  422,722 wamefaulu katika mitihani wa kidato  cha  nne huki wasichana waliofaulu ni 175,296  sawa na asilimia  79.46 na wavulana ni 165,618 sawa na asilimia 81.94 na kwamba ubora wa ufaulu unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa  135,301 sawa na asilimia 32.01 walipata daraja la kwanza hadi la tatu ambayo wasichana ni 58,542 sawa na asilimia 26.54  na wavulana  ni 76,759 sawa na asilimia  37.97.

"Takwimu za matokeo zinaonesha watahiniwa wamefanya vizuri katika masomo mengi ya msingi ambayo ufaulu wa masomo hayo uko juu ya wastani kati ya asilimia  51.25 na 91.31. Lakini hawakufanya vizuri katika masomo ya Fizikia na Hisabati licha  ya ufaulu wa fizikia kuimarika kutoka asilimia 45.50 kwa mwaka 2018 hadi asilimia  48.38 2019," amesema Dk Msonde.

Akitaja Shule 10 bora Kitaifa katika mitihani wa kidato cha nne  ni Kemebos (Kagera), Mtakatifu Francis  (Mbeya), Feza Boy's  na Canossa (Dar es Salaam), Shule ya Wasichana Anwarite (Kilimanjaro), Precious  Blood (Arusha), Marian Boys' Mtakatifu Augustine Tagaste (Dar es Salaam), Maua Seminari  (Kilimanjaro  na Musabe Boys (Mwanza).

Watahiniwa 10 bora Kitaifa ni Joan Ritte (Mtakatifu  Francis), Denis Kinyange (Nyegezi  Seminari), Erick Mutasingwa (Sengerema  Seminari), Rosalia Mwidege (Mtakatifu  Francis), Domina Wamara (Mtakatifu Francis), Mvano Cabangoh (Feza Boys') , Agatha Mlelwa, Sarah Kaduma na Shammah Kiunsi (wote Mtakatifu Francis) na Lucy Magashi (Huruma Girls).

Dk Msonde  aliwataja wasichana 10 bora ni Joan Ritte, Rosalia Mwidege, Domina Wamara, Agatha Mlelwa, Sarah Kaduma, Shammah Kiunsi wote kutoka Shule ya Mtakatifu Francis, Lucy Magashi (Huruma Girls), Imani Sanga, Joyce Magwaza na Marther Ngowi (Mtakatifu Francis  Mbeya).

Wavulana 10  bora Kitaifa  ni  Kinyange (Nyegezi Seminari),  Mutasingwa (Sengerema  Seminari), Cabangoh (Feza Boys'), Yohana Mwashambwa (Malangali- Iringa), Bruno Bruno (Don Bosco Seminari  Iringa), Nelson Mbigili (St Dominic Savio-Iringa), Ebenezer  Mujungu (Faraja Seminari  ya Kilimanjaro), Timothy  Mjuni, Richardson Kwareh na Henry  Kimbori wote kutoka Centennial  Seminari  za Mkoa wa Pwani.

Pia alitaja Mikoa mitatu iliyofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha nne  ambayo ni Kilimanjaro, Arusha na Iringa wakati hakuna mikoa iliyoshuka ufaulu kwa  miaka mitatu mfululizo.

Dk Msonde amesema halmashauri 10 zilizofanya vizuri katika mitihani huo ni Bagamoyo mkoani Pwani yenye shule 19, Bukoba mkoani Kagera, Meru mkoani Arusha, Mafinga mkoani Iringa, Kibaha mkoani Pwani, Njombe mkoani Njombe, Kibondo mkoani Kigoma, Kahama mkoani Shinyanga , Moshi mkoani Kilimanjaro  na Bariadi mkoani Simiyu.

Ameaema halmashauri zilizoongeza ufaulu kwa miaka mitatu mfululizo  ni Madaba na Mbinga za mkoani Ruvuma, Mafinga (Iringa), Bukoba (Kagera) Mpimbwe (Katavi), Pangani (Tanga), Kasulu (Kigoma), Iringa (Iringa), Njombe (Njombe) na Kilolo (Iringa).

Aidha amezitaja halmashauri kumi zilizoshuka ufaulu kwa miaka 3 mfululizo kuwa ni, Mafia (Pwani), Kibiti (Pwani), Geita (Geita), Kakonko (Kigoma), Kondoa (Dodoma), Mpanda (Katavi), Kishapu ( Shinyanga), Kiteto (Manyara), Bumbuli (Tanga) na Malinyi (Morogoro).

"Takwimu za matokeo ya mitihani ya maarifa (QT) zinaonesha kuwa jumla ya watahiniwa  7,070 sawa na asilimia  62,09 ya watahiniwa  11,386 wamefaulu mitihani  hiyo. NECTA imefuta mitihani  kwa watahiniwa  333 waliofanya udanganyifu katika mitihani  ya kidato cha nne na kati ya watahiniwa  waliofanya udanganyifu 142 wa mitihani  ya darasa la nne, 29 wa kidato cha pili na 162 wa kidato cha nne," amefafanua Dk Msonde.

Ameongeza kuwa baraza hilo limezuia kutoa matokeo ya watahiniwa  538 ambao walipata matatizo ta kiafya na kushindwa kufanya upimaji wa masomo yote au mdai kubwa ya masomo na kwamba wanaruhusiwa kufanya mitihani  hiyo kwa mwaka 2020 kwa mujibu wa kanuni za mitihani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza hilo, Charles Msonde

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...