Shirikisho la Soka barani Afrika (Caf) watatoa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2019, leo Jumanne katika sherehe zitakazofanyika nchini Misri katika eneo la ufukwe la Hurghada.

Nyota wa Algeria na Manchester City Riyad Mahrez atakuwa akichuana na nyota wengine wawili wa Liverpool Sadio Mane wa Senegal na Mohamed Salah kutoka Misri.

Mane na Salah waliisadia klabu yao ya Liverpool kutwaa ubingwa wa Ulaya na kombe la dunia la vilabu.

Mahrez aliiongoza Algeria akiwa nahodha katika michuano ya kombe la mataifa ya Africa yaliyofanyika mwaka jana nchini Misri.

Hatua ya mwisho ya upigaji kura kwa tuzo za wanaume Na wanawake,watachaguliwa na makocha wakuu/ Wakurugenzi wa ufundi na manahodha wa timu za taifa.

Wachezaji wa kiume wanawania tuzo
Ni:
Mohamed Salah (Egypt & Liverpool)

Riyad Mahrez (Algeria & Manchester City)

Sadio Mane (Senegal & Liverpool)

Wanaowania kwa upande wa wanawake

Ajara Nchout (Cameroon & Valerenga)

Asisat Oshoala (Nigeria & Barcelona)

Thembi Kgatlana (South Africa & Beijing Phoenix FC).
.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...