Kikao
kazi cha Kupitia ,Kuboresha na Kuhuisha Rasimu ya Mpango Kabambe wa
Matumizi ya Ardhi ya Kilimo wa mwaka 2020 kimefanyika mjini Morogoro leo
kwa lengo la wajumbe kutoa maoni yao ya kuuboresha .
Akizungumza
wakati wa kikao kazi hicho Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa Ardhi ya
Kilimo Sospeter Mtemi amesema lengo la wizara ni kupata maoni ya wadau
ili kuwa na mpango kabambe wa kuhakikisha ardhi ya kilimo inalindwa na
kutumika kwa mujibu wa sheria kukuza sekta ya kilimo.
"
Kukamilika kwa kazi hii kutaifanya serikali kuwa na mpango kabambe wa
kwanza nchini wa matumizi bora ya ardhi utakaotumika na taasisi zote za
umma na binafsi kusimamia shughuli za kilimo" alisema Mtemi
Msisitizo
unawekwa kwenye kukifanya kilimo kuchangia upatikanaji wa uhakika wa
chakula ,biashara na kukuza ajira kwa watanzania kupitia mpango kabambe
unaoandaliwa.
Kikao kazi
kimeazimia kuwa rasimu ya mpango kabambe iwasilishwe kwa wadau wengi
zaidi ili watoe maoni yao kabla ya kikao kingine kuitishwa.
Mchakato huu ulianza mwaka 2009 lakini ukasitishwa kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha kuukamuilisha.
Kikao
kazi hiki kiliandaliwa na wizara ya Kilimo na kushirikisha wizara zote
za kisekta ikiwemo ,Mifugo na Uvuvi,Ofisi ya Makamu wa
Rais-Mazingira,Ofisi ya Rais Tamisemi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara ya
Ardhi,Wizara ya Maliasili na utalii na sekta binafsi wakiwemo MVIWATA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...