Afisa Maendeleo ya Jamii Kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bw. Matias Haule akiongea na wanafunzi wa Bai Sekondari wakati wa Kampeini ya kupambana na VVU kwa vijana jana wilayani hapo Mkoani Dodoma.
Wanafunzi wa Bai Sekondari wakifuatilia jambo  wakati wa Kampeini ya kupambana na VVU kwa vijana jana wilayani hapo Mkoani Dodoma.
*****************************
Serikali imetaja vichocheo vinavyochangaia maambukizi ya VVU kwa kundi la wasichana na wavulana kuwa ni kutokana na baadhi ya vijana kutopenda kufanya kazi halali za kujipoatia kipato na hivyo kuendekeza biashara ya ngono kama njia nyepesi ya kujipatia mahitaji muhimu.
Akiongea na baadhi ya Wazee Maarufu pamoja na baadhi ya viongozi wa dini  Wilayani Bai Mkoani Dodoma  jana Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu Bw. Matias Haule alitaja Maudhui mabaya ya picha zisizofaa kuwa pia kichocheo cha Maambukizi hayo.
Bw. Haule aliitaja mitandao ya Kijamii kama vile twitter, Whats App pamoja na Instagram kuwa inachukua muda mwingi wa vijana na muda wote unatumika kufuatilia matendo ya ngono hivyo kuchochea maambukizi na kupelekea hata kupata udhalilishaji wa kingono mtandaoni.
Afisa huyo pia aliitaja mikesha na ngoma za usiku kama vile midundiko na vigodolo kupigwa marufuku katika Jamii kwasababu sherehe hizi uwavutia vijana wengi zaidi ambao kwa sasa wanapata maabukizi yz VVU kwa wingi kuliko makundi mengine katika Jamii.
Aidha Bw. Haule amutaja uelewa mdogo wa maabukizi ya VVU kwa vijana  na baadhi yao kutozingatia maelekezo ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI ikiwemo matumizi mabaya ya kondomu ni sababu kubwa inayochangia vijana wengi kwa sasa kutumbukia katika janga la UKIMWI.
Bw. Haule hakuwaacha mbali wazazi na walezi kwani ameonya kuwa wazazi wanachangia katika malezi mabovu ya vijana kwa kushindwa kutoa ulinzi kwa vijana hasa wa kike na kuwashawishi kuijiingiza katika ngono zembe,ubakwaji na ulawiti.
Wizara ya Afya Maendealeo ya Jamii kwa Kushirikiana na TACAIDS pamoja na Shirika la TASAF wako Mkoani Dodoma kutembelea wasichana barehe na wanawake vijana pamoja na Shule mbalimbali Mkoani humo kwa lengo la kuhamasisha vijana juu yatishio jipya la maambukizi ya UKIMWI kwa vijana na zoezi hili litaendelea kwa Mkoa wa Morogoro na baadae Nchi Nzima.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...