Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
 Tanzania (TRA) Dkt. Edwin Mhede akizungumza na waandishi wa habari 
jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) wakati akitangaza makusanyo ya 
kodi ya kipindi cha Robo ya Pili ya mwaka 2019/20 ambapo amesema kwa 
mara nyingine, TRA imevunja rekodi kwa kukusanya jumla ya kiasi cha sh. 
trilioni 1.987 kwa mwezi Desemba 2019 sawa na ufanisi wa asilimia 100.20
 kutoka katika lengo la kukusanya kiasi cha sh. trilioni 1.983 kwa mwezi
 huo. Kulia kwake ni Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Bw. Msafiri 
Mbibo.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
 Tanzania (TRA) Dkt. Edwin Mhede akizungumza na waandishi wa habari 
jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) wakati akitangaza makusanyo ya 
kodi ya kipindi cha Robo ya Pili ya mwaka 2019/20 ambapo amesema kwa 
mara nyingine, TRA imevunja rekodi kwa kukusanya jumla ya kiasi cha sh. 
trilioni 1.987 kwa mwezi Desemba 2019 sawa na ufanisi wa asilimia 100.20
 kutoka katika lengo la kukusanya kiasi cha sh. trilioni 1.983 kwa mwezi
 huo. Kulia kwake ni Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Bw. Msafiri 
Mbibo na kushoto kwake ni Kamishna wa Idara ya Walipakodi Wakubwa Bw. 
Alfred Mregi.
******************************
Na Veronica Kazimoto
Dar es Salaam.
Mamlaka
 ya Mapato Tanzania (TRA), kwa mara nyingine, imevunja rekodi kwa 
kukusanya jumla ya kiasi cha sh. trilioni 1.987 kwa mwezi Desemba 2019 
ambayo ni rekodi ya kwanza kufikiwa tangu kuanzishwa kwake 
ikilinganishwa na rekodi ya mwezi Septemba, 2019 iliyokuwa sh. trilioni 
1.767.  
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa 
Mamlaka hiyo Dkt. Edwin Mhede amesema kuwa, makusanyo hayo ya mwezi 
Desemba 2019 ni sawa na ufanisi wa asilimia 100.20 kutoka katika lengo 
la kukusanya kiasi cha sh. trilioni 1.983 kwa mwezi huo.
“Ni 
kweli kwamba, kitaalam, miezi tofauti hailinganishiki moja kwa moja. 
Hata hivyo, kwa makusanyo haya ya sh. trilioni 1.987 kwa mwezi Desemba 
2019, TRA imevunja rekodi yake yenyewe iliyoiandika mwezi Septemba 2019 
ambapo ilikusanya jumla ya sh. trilioni 1.767 ikiwa ni sawa na asilimia 
97.20 ya lengo la kukusanya sh. trilioni 1.817 katika kipindi hicho,” 
alisema Dkt. Mhede.
Akizungumzia
 makusanyo ya kipindi cha Robo ya Pili ya mwaka 2019/20 inayohusisha 
mwezi Oktoba, Novemba, na Desemba yenyewe, Kamishna Mkuu Mhede amesema 
kuwa, TRA imefanikiwa kukusanya jumla ya sh. trilioni 4.972 sawa na 
ufanisi wa asilimia 97.49 ya lengo la kukusanya jumla ya sh. trilioni 
5.100.
“Makusanyo
 haya ya robo ya pili ya mwaka 2019/20 ni sawa na ukuaji wa asilimia 
19.78 ikilinganishwa na kipindi kama hiki cha Robo ya Pili ya mwaka 
2018/19 ambapo Mamlaka ilikusanya sh. trilioni 4.151 ikiwa ni sawa na 
ufanisi wa asilimia 87.59 kutokana na lengo la kukusanya mapato kiasi 
cha sh. trilioni 4.739 katika kipindi hicho,” alifanunua Kamishna Mkuu 
Mhede.
Ameeleza
 kuwa, kwa upande wa makusanyo ya mapato ya Serikali kwa mwezi Oktoba 
2019, TRA ilikusanya kiasi cha sh. trilioni 1.484 na Novemba 2019, 
Mamlaka ilikusanya sh. trilioni 1.501 sawa na ufanisi wa asilimia 93.98 
na asilimia 97.59 kutoka katika malengo ya kukusanya sh. trilioni 1.579 
na sh. trilioni 1.538 kwa mwezi Oktoba na Novemba 2019.
Kamishna
 Mkuu Mhede ameongeza kuwa, makusanyo hayo ni muendelezo wa kiashiria 
cha wazi kwamba Walipakodi na Watanzania walio wengi wameendelea 
kuelewa, kukubali, na kuitikia wito wa Serikali ya Awamu ya Tano wa 
kuongeza mapato ya ndani kwa ajili ya maendeleo ya Taifa zima. 
“Kwa 
kuwa Walipakodi wengi wameitikia wito wa kulipa kodi kwa mujibu wa 
Sheria, ni rai yangu kwamba asiwepo mlipakodi hata mmoja ambaye 
atathubutu kubaki nyuma. Ni busara wafanyabiashara wote wakaungana na 
kundi kubwa la Washindi, yaani, kundi kubwa la wanaolipa kodi kwa hiari,
 kwa ukamilifu, na kwa wakati, alisisitiza Dkt. Mhede.
Pia, 
amewashukuru walipakodi waliolipa kodi kwa wakati na hivyo kupelekea 
kuongezeka kwa makusanyo ambayo yatapelekea utekelezaji wa miradi 
mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.
“Kwa 
namna ya kipekee, napenda kuwashukuru Walipakodi wote waliolipa kodi ya 
Serikali na kupelekea Mamlaka kufikia makusanyo haya ya kihistoria kwa 
mwezi Desemba 2019. Pia, tunaishukuru sana Serikali ikiwa ni pamoja na 
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, 
Taasisi za Maendeleo, na Sekta Binafsi kwa kuendelea kuipatia TRA 
ushirikiano stahiki katika kutekeleza majukumu yake ya kukadiria, 
kukusanya, na kuhasibu mapato ya Serikali,” Alisema Kamishna Mkuu Mhede.
Aidha,
 ametoa wito kwa wamiliki wote wa majengo nchini kujitokeza kulipia kodi
 za majengo ili kuepuka usumbufu wa kulipa mwishoni mwa mwaka wa fedha 
2019/2020 ambapo amesema kuwa, kwa sasa viwango ni rafiki na vinalipika 
kwa urahisi.
Amevitaja
 viwango hivyo kwa mwaka kuwa ni sh. 10,000 kwa nyumba ya kawaida, sh. 
50,000 kwa kila sakafu ya nyumba ya ghorofa katika Majiji, Manispaa, na 
Halmashauri za Miji, na sh. 20,000 kwa jengo la ghorofa katika maeneo ya
 Halmashauri za Wilaya.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...