Na Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha

Wafanyabiashara wa soko la Samunge mkoani Arusha wameiomba halmashauri ya jiji la Arusha kuwaboreshea miundombinu ya soko hilo ikiwemo mitaro ambayo imekuwa ikitiririsha maji machafu hasa kipindi cha mvua.

Aidha wamesema kuwa,wanaomba  uongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha unawasaidia kutatua kero hiyo kwani wapo hatarini kukumbwa na magonjwa ya milipuko hasa kipindi hiki Cha mvua .

Suzan Mollel Mmoja wa Wafanyabiashara katika soko hilo,amesema kuwa  kwa muda mrefu Sasa wamekuwa wakiuza bidhaa zao katika soko hilo huku miundombinu ikiwa sio rafiki kwa afya za walaji.

Alisema kuwa,kipindi cha mvua  soko hilo limekuwa likifurika maji machafu katika mtaro uliopo eneo hilo ambapo maji hayo husababisha usumbufu mkubwa kwa wafanyabiashara hao na wanunuzi kutokana na kutoa harufu kali .

"tunaomba sana jamani tuboreshewe mazingira ya soko hili kwa kututengenezea miundombinu hasa mitaro ambayo imekuwa ikitiririsha maji machafu kipindi cha mvua na kutoa harufu kali na hivyo kuhatarisha afya za watumiaji."alisema Suzan.

Naye Mfanyabiashara mwingine ,Anita Emmanuel alisema kuwa,swala la kutengenezewa miundombinu ya soko hilo limekuwa la muda mrefu sana,lakini limekuwa halipatiwi ufumbuzi na hivyo kuhatarisha afya za walaji na wafanyabiashara hao kwa ujumla.

Alisema kuwa,wanaomba kero hiyo kupatiwa ufumbuzi wa haraka hasa katika kipindi hiki cha masika kwani ili kuwawezesha kufanya biashara zao katika sehemu iliyo bora na salama .

Elizabeth Mushi Mmoja wa Wafanyabiashara katika soko hilo,alisema kuwa,wanaomba uongozi wa halmashauri hiyo kuingilia Kati swala la utengenezaji wa miundombinu hiyo hasa ya mitaro kwani kipindi cha mvua yamekuwa yakifunguliwa maji machafu  ya chooni  ambayo hutiririka kwenye bidhaa zao na kuwazuia kufanya biashara.

Mushi alisema kuwa,kipindi cha mvua wamekuwa wakishindwa kufanya biashara katika soko hilo kutokana na maji machafu yanayopita kwenye mtaro huo kwenda kwenye bidhaa zao na hivyo kuhatarisha afya za walaji.

Hata hivyo Michuzi Globu ilipojaribu kumtafuta Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha ,hakupatikana kwenye simu ili kuzungumzia swala hilo.
Picha ikionyesha mfanyabiashara Wa ndizi wakiwa wanamuuzia ndizi mteja wao katika maeneo ya  Leganga ,wilayani Arumeru  (picha na Woinde Shizza, Arusha)
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...