Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema Ofisi ndogo za NIDA iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imeibiwa vifaa vyote na Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo.
Muro amesema kuwa wizi huo umefanyika kimtandao kwa sababu ofisi ndogo za NIDA zipo karibu kabisa na jengo la NMB Bank na halmashauri ina walinzi wake.
Aidha ametaja vifaa vilivyoibwa ni pamoja na Kompyuta Mpakato nne na Kamera si chini ya tatu pamoja na vifaa vingine vilivyokuwa vikiingiza majina kwenye mifumo na ambapo amesema wizi huo unaonekana ni wa ndani kwani milango haikuvunjwa.
Ameongeza kuwa tukio hilo limewashtua na ni mara ya pili tukio kama hilo kutokea amapo mara ya kwanza lilitokea Ofisi za NIDA Makao Makuu Wilaya ya Arumeru na baadhi ya vifaa viliibwa taratibu kwa muda mrefu.
Katika hatua nyingine Jerry Muro amewaomba Wananchi kuwa, watulivu kwa kipindi hiki ambacho yeye na Kamati ya Ulinzi na Usalama wanaendelea kufuatia na vile vile ameeleza kuwa kwa sasa hakutakuwa na huduma katika Ofisi hiyo ya Halmashauri ya Arusha.
Muro amesema kuwa wizi huo umefanyika kimtandao kwa sababu ofisi ndogo za NIDA zipo karibu kabisa na jengo la NMB Bank na halmashauri ina walinzi wake.
Aidha ametaja vifaa vilivyoibwa ni pamoja na Kompyuta Mpakato nne na Kamera si chini ya tatu pamoja na vifaa vingine vilivyokuwa vikiingiza majina kwenye mifumo na ambapo amesema wizi huo unaonekana ni wa ndani kwani milango haikuvunjwa.
Ameongeza kuwa tukio hilo limewashtua na ni mara ya pili tukio kama hilo kutokea amapo mara ya kwanza lilitokea Ofisi za NIDA Makao Makuu Wilaya ya Arumeru na baadhi ya vifaa viliibwa taratibu kwa muda mrefu.
Katika hatua nyingine Jerry Muro amewaomba Wananchi kuwa, watulivu kwa kipindi hiki ambacho yeye na Kamati ya Ulinzi na Usalama wanaendelea kufuatia na vile vile ameeleza kuwa kwa sasa hakutakuwa na huduma katika Ofisi hiyo ya Halmashauri ya Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...