klabu ya Yanga Sc imetangaza usajili wa mchezaji raia wa Ghana, Bernard Morrison mwenye umri wa miaka  26, kutoka klabu ya DC Motema Pembe ya nchini DRC Congo.

Takwimu za Morrison: Ligi kuu Afrika Kusini amecheza michezo 18 na kufunga mabao mawili, ligi kuu Ghana katika michezo 16 ametikisa nyavu mara 6.

Mchezaji huyo anamudu kucheza nafasi mbalimbali uwanjani katika safu ya ushambuliaji, mshambuliaji wa kati na mshambuliaji wa pembeni akitokea kulia ama kushoto.

Bernard amewahi kuchezea timu kadhaa kabla ya kutua Jangwani katika dirisha hili dogo la usajili, amepita As Vita, Dc Motema Pembe, Ashanti ya Ghana na Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

Imeandikwa na @abasi_shabani_17

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...