Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo nchini Tanzania, Profesa Elisante Ole Gabriel amesema wanatarajia kuanzisha kliniki za kutoa ushauri wa ufugaji katika kila Halmashauri ili kuongeza thamani ya ngozi inayozalishwa.
Profesa Gabriel ameyasema hayo leo Jumamosi Machi 7, 2020 wakati wa kufungua mkutano wa wadau mbalimbali wa sekta Mifugo jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Mkutano huo ni vyama vya Wafugaji Kuku Nguruwe pamoja na wadau wa ngozi uliolenga kupokea changamoto za katika Biashara Biashara ili zitafutiwe ufumbuzi.
Profesa Ole Gabriel amesema kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanunuzi kuwa kuna baadhi ya ngozi haikidhi viwango vya ubora unaotakiwa katika uzalishaji bidhaa jambo ambalo limekuwa likiikosesha serikali mapato.
“Sasa ili kukabiliana na suala hili, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Tawala za Mitaa (Tamisemi) tutashirikiana katika hatua mbalimbali ili kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na kliniki ya mifugo,” amesema Profesa Ole Gabriel.
Profesa Ole Gabriel amesema katika sehemu ya mfugaji ataweza kupata elimu ya namna ya kutunza mifugo yake huku akitolea mfano wa ng’ombe kuanzia akiwa na mimba, baada ya kuzaa na namna ya kumtunza hadi anakuwa mkubwa ili aweze kuleta faida inayokusudiwa na wafugaji pamoja na serikali kupata mapato sitahiki.
“Suala la utunzaji wa mifugo inayozalisha ngozi litaenda hadi katua za uchinjaji ambapo visu maalumu vitasambazwa katika maeneo na elimu maalumu ya uchunaji na elimu italolewa inayozingatia viwango vya upatikanaji ngozi bora,” amesema
Mwenyekiti wa Wadau wa ngozi Tanzania, Adam Ngamilo ameonyesha kufurahishwa na uamuzi wa serikali huku akibainisha kuwa utawasaidia katika kuboresha mnyororo wa thamani za bidhaa.
“Suala hili lilikuwa ni changamoto sana kwetu hasa sisi viongozi tunaomaliza muda tunaamini watakaoingia wataitumia ipasavyo,” amesema Ngamilo
Kwa upande wa wafugaji wa kuku wameiomba Serikali kuwasaidia kupata mitaji ili waweze kufanikisha malengo yao.
“Tunaiomba Serikali itusaidie kupata mitaji ambayo kupitia mikopo ya riba nafuu ili tuweze kufika mbali na kutoa fursa za ajira kaa watu wengi zaidi,” amesema Denis Joseph ambaye ni mfugaji wa kuku
Akijibu hoja hiyo, Katibu mkuu huyo amesema atahakikisha pia anazungumza na katibu mkuu wa Tamisemi ili asilimia kumi inayotengwa katika kila halmashauri iweze kunufaisha wafugaji wadogo ikiwamo wakina mama na vijana.
Kwa sasa sheria inazitaka halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ili kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake asilimia nne, vijana asilimia nne na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu.
Profesa Gabriel ameyasema hayo leo Jumamosi Machi 7, 2020 wakati wa kufungua mkutano wa wadau mbalimbali wa sekta Mifugo jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Mkutano huo ni vyama vya Wafugaji Kuku Nguruwe pamoja na wadau wa ngozi uliolenga kupokea changamoto za katika Biashara Biashara ili zitafutiwe ufumbuzi.
Profesa Ole Gabriel amesema kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wanunuzi kuwa kuna baadhi ya ngozi haikidhi viwango vya ubora unaotakiwa katika uzalishaji bidhaa jambo ambalo limekuwa likiikosesha serikali mapato.
“Sasa ili kukabiliana na suala hili, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Tawala za Mitaa (Tamisemi) tutashirikiana katika hatua mbalimbali ili kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na kliniki ya mifugo,” amesema Profesa Ole Gabriel.
Profesa Ole Gabriel amesema katika sehemu ya mfugaji ataweza kupata elimu ya namna ya kutunza mifugo yake huku akitolea mfano wa ng’ombe kuanzia akiwa na mimba, baada ya kuzaa na namna ya kumtunza hadi anakuwa mkubwa ili aweze kuleta faida inayokusudiwa na wafugaji pamoja na serikali kupata mapato sitahiki.
“Suala la utunzaji wa mifugo inayozalisha ngozi litaenda hadi katua za uchinjaji ambapo visu maalumu vitasambazwa katika maeneo na elimu maalumu ya uchunaji na elimu italolewa inayozingatia viwango vya upatikanaji ngozi bora,” amesema
Mwenyekiti wa Wadau wa ngozi Tanzania, Adam Ngamilo ameonyesha kufurahishwa na uamuzi wa serikali huku akibainisha kuwa utawasaidia katika kuboresha mnyororo wa thamani za bidhaa.
“Suala hili lilikuwa ni changamoto sana kwetu hasa sisi viongozi tunaomaliza muda tunaamini watakaoingia wataitumia ipasavyo,” amesema Ngamilo
Kwa upande wa wafugaji wa kuku wameiomba Serikali kuwasaidia kupata mitaji ili waweze kufanikisha malengo yao.
“Tunaiomba Serikali itusaidie kupata mitaji ambayo kupitia mikopo ya riba nafuu ili tuweze kufika mbali na kutoa fursa za ajira kaa watu wengi zaidi,” amesema Denis Joseph ambaye ni mfugaji wa kuku
Akijibu hoja hiyo, Katibu mkuu huyo amesema atahakikisha pia anazungumza na katibu mkuu wa Tamisemi ili asilimia kumi inayotengwa katika kila halmashauri iweze kunufaisha wafugaji wadogo ikiwamo wakina mama na vijana.
Kwa sasa sheria inazitaka halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ili kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake asilimia nne, vijana asilimia nne na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa Elisante Ole Gabriel
akizungumza wakati wa mkutano vyama vya wafugaji kuku na nguruwe
uliolenga kupokea changamoto ili zitafutiwe ufumbuzi kilichofanyika
katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wadau wa Kuku Tanzania, Harko Bhagat akitoa
changamoto tatu wanaziozipata kwenye ufugaji wa kuku kwa Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel(hayupo pichani)
wakati wa mkutano vyama vya wafugaji kuku na nguruwe pamoja uliolenga
kupokea changamoto ili zitafutiwe ufumbuzi uliofanyika katika ukumbi wa
Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Makamu
Mwenyekiti wa TAPIFADorin Maro akitoa changamoto wanazokutana nazo
kwenye ufugaji wa Nguruwe kwa wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na
Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel(hayupo pichani) wakati wa mkutano vyama
vya wafugaji kuku na nguruwe uliolenga kupokea changamoto ili
zitafutiwe ufumbuzi uliofanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar
es Salaam leo.
Baadhi
ya wafugaji wa kuku na nguruwe pamoja na wauzaji wa vyakula vya mifugo
wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole
Gabriel alipokuwa anafungua mkutano vyama vya wafugaji kuku na nguruwe
uliolenga kupokea changamoto ili zitafutiwe ufumbuzi.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel(katikati)
akizungumza wakati wa kufungua mkutano wadau wa ngozi uliolenga kuchagua
viongozi wapya wa Chama hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Wizara
hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wadau wa
ngozi Tanzania, Adam Ngamilo.
Baadhi
ya wadau wa ngozi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na
Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel alipokuwa anafungua mkutano kwa ajili
ya kuchagua uongozi mpya
Aliyekuwa
Mwenyekiti wa Wadau wa ngozi Tanzania, Adam Ngamilo akizungumza wakati
wa mkutano wa wadau wa ngozi waliokutana kwa ajili ya kuchagua uongozi
mpya. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante
Ole Gabriel.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel akiwa
kwenye picha ya pamoja na wadau wa Ngozi mara baada ya kufungua mkutano
wao uliokuwa unahusu kuchagua uongozi mpya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...