NA MWAMVUA MWINYI,BAGAMOYO
 
Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa amekabidhi viti mwendo kwa watoto wenye ulemavu wa miguu katika jimbo lake.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi viti mwendo hivyo, Dkt. Kawambwa alisema kuwa, viti mwendo hivyo ni msaada kutoka kwa mama Janeth Magufuli hivyo anakabidhi kwa walengwa ili kutimiza wajibu wake kama alivyooagizwa na mama Janeth Magufuli.
 
Alisema Viti mwendo hivyo vitawasaidia watoto hao kutembea sehemu mbali mbali kwa kuendesha wenyewe au kuendeshwa na kuondoa usumbufu wa kuwabeba hata pale wanapokuwa na safari za lazima kama vile Hospitali Nk. 
 
Aidha, aliwataka wazazi na walezi kuvitunza vifaa hivyo ili viendelee kuwahudumia watoto hao kwa muda mrefu zaidi jambo ambalo litampa moyo yule aliyetoa na kufikiria kutoa msaada mwingine.
 
Katika hatua nyingine Mbunge huyo wa Jimbo la Bagamoyo aliwashauri kina mama wenye watoto walemavu kuunda kikundi na kukisajili ili waweze kupatiwa mikopo ya serikali inayotolewa kwa vikundi.
 
Alisema serikali haiwezi kusaidia wananchi mmoja mmoja hivyo ni vyema wakiwa kwenye kikundi ili waweze kupata mikopo inayotolewa na Halmashauri ambayo haina riba na kwamba itawasaidia kujiendeleza kulingana malengo watakayojiwekea.
 
Dkt. Kawambwa alitoa rai hiyo baada ya kina mama wenye watoto walemavu kumuomba awasaidie wapate mitaji kwa ajili ya biashara ili kukabiliana na malezi ya watoto hapo.
Kwa upande wao wazazi na walezi wa watoto hao walimshukuru Mbunge huyo kwa kufikisha viti hivyo kama alivyokabidhiwa na mama Janeth Magufuli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...