Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha (DVC(AF) Prof. Ernest Kihanga akitoa ufafanuzi kwa Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya Madarasa, mradi mpya ambao unahusisha ujenzi wa vyumba vya madarasa, kumbi za mikutano na ofisi za watumishi, eneo la Maekani Chuo Kikuu Mzumbe.
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha (DVC(AF) Prof. Ernest Kihanga akitoa  maelezo kwa Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kuhusu ujenzi wa Mabweni unaotarajiwa kumalizika kabla ya Juni 2020; wenye thamani ya TSh. Bil 6.5 Maekani Kampasi Kuu.
 Baadhi ya Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakiwasili eneo la Maekani kunakojengwa Hosteli za kisasa za Chuo Kikuu Mzumbe. Fedha za Ujenzi zimetolewa na Serikali ya Awamu ya Tano. 
 Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha (DVC(AF) Prof. Ernest Kihanga mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa mabweni ya kisasa Maekani, mradi unaofadhiliwa na Serikali ya Awamu ya Tano.
 Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakitembea kuelekea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hosteli za kisasa Maekani Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi Kuu.
Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakiwa kwenye ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe walipowasili kutembelea maendeleo ya miradi inayotekelezwa kwa ufadhili wa Serikali. Maafisa hao wa Mkoani Morogoro kushiriki kikao kazi kinacholenga kutangaza mafanikio ya Wizara.


======  ========  =======

Maafisa Mawasiliano toka Taasisi na Vyuo Vikuu vya Umma vilivyopo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, wametembelea miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Awamu ya Tano , Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi Kuu.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha (DVC(AF) Prof. Ernest Kihanga, akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo hicho amesema, mpaka sasa maendeleo ya ujenzi wa mabweni unaendelea vema na unatarajiwa kukamilika mapema mwezi Juni mwaka huu 2020.

“Tunashukuru sana Serikali kuona umuhimu mkubwa wa kuwekeza kwenye ujenzi wa Mabweni, tunaimani kubwa baada ya mradi huu kukamilika zaidi ya vijana 1000 watapata malazi na hivyo tutadahili wanafunzi wengi zaidi wanaomaliza shule na kukosa nafasi kwenye vyuo vyetu” alisema

Mbali na mradi wa ujenzi wa mabweni, Chuo hicho kinaendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa, kumbi za mikutano na ofisi za Watumishi ambapo kukamilika kwa jengo hilo kutawezesha vijana zaidi ya 1000 kushiriki masomo kwa mara moja. Mradi huo unakusudiwa kukamilika mwezi Juni 2020.

Mradi wa Ujenzi wa mabweni unafadhili na Serikali ya Awamu ya Tano kwa Tshs. Bil 6.5 wakati ujenzi wa vyumba vya madarasa na kumbi za mikutano unategemea mapato ya ndani na utagharimu takribani Tshs. Bil 3.5

Wakizungumza mara baada ya ziara hiyo; maafisa hao wameonyesha kufurahishwa na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali kupitia Taasisi zake, na kwamba hatua hiyo itawezesha watanzania wengi kujiunga na Elimu ya juu nchini inayotolewa na Vyuo vya Umma.

Maafisa Mawasiliano wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wako mkoani Morogoro kushiriki kikao kazi kilicholenga kupanga mikakati ya uhamasishaji na Elimu kwa Umma kuhusu shughuli zinazofanywa na kusimamiwa na Wizara hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...