Marekani imeeleza kufurahishwa na mafanikio ya Tanzania katika masuala ya ushirikishwaji wa wanawake katika ngazi za uongozi wa kisiasa na maamuzi na hatua zilizochukuliwa kuhakikisha wanawake na wasichana wanapata elimu bora na salama.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na mshauri wa Rais Trump kuhusu masuala ya maendeleo ya wanawake Balozi Kelley Currie mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Washington.

Mara baada ya kukutana na mshauri huyo wa Rais Trump kuhusu masuala ya maendeleo ya wanawake Balozi Kelley Currie Prof. Kabudi pia amekutana na kufanya mazungumzo na kundi la Washington Intergovermental Professionals Group wakiwemo maseneta na mabalozi kutoka nchi mbalimbali waliopo Marekani kwa lengo la kuwaelezea fursa za uwekezaji zilizopo nchini.

Balozi wa Tanzania Nchini Marekani Balozi Willson Masilingi kwa upande wake amesema ziara ya Prof. Kabudi nchini Marekani kwa kiasi kikubwa imesaidia kuendelea kuimarisha mahusiano baina ya Tanzania na Marekani na kwamba nafasi ya kukutana na makundi mbalimbali yatahamasisha wawekezaji wengi marekani kwenda Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...