Vipaumbele
hivyo vinavyotajwa kuleta mapinduzi makubwa, vinalenga kutafuta suluhu dhidi ya
changamoto za mapambano ya kutokomeza malaria. Changamoto hizi zinajumuisha;
ushiriki hafifu wa wanawake, watoto na vijana, uhaba wa fedha toka sekta za
ndani, za umma na binafsi pamoja na tishio la kudumaa kwa michango ya wahisani.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Mheshimiwa Kenyatta alitangaza, “Pamoja na mafanikio
makubwa yaliyopatikana kwenye vita hii ndani ya miaka kumi iliyopita, ili kuwa
na Afrika Tunayoitaka kama
ilivyoelezwa kwenye Mpango wa 2063,
tusijisahau, badala yake tutafute na kupata raslimali zaidi zitakazotusaidia
kutokomeza malaria na kuokoa maisha. Na ndiyo maana tumeainisha maeneo ya
vipaumbele yatakayokuwa msingi wa utendajikazi wangu kama mwenyekiti wa ALMA:
1. Matumizi ya dijitali na takwimu
Uanzishwaji
wa majukwaa ya kidijitali yanayofika katika mataifa mbalimbali ili kusaidia
upatikanaji na uwazi wa takwimu za mapambano dhidi ya malaria. Hii itasaidia
kwa kiwango kikubwa juhudi zetu hasa katika maeneo yaliyoathirika zaidi. Mbinu
hii itasaidia pia kuwa na tafiti za ndani ya Afrika hasa kwa kutumia taasisi za
kitafiti zilizopo tayari ndani ya Afrika. Kwa kuimarisha upatikanaji wa
takwimu, wananchi wote watakuwa na uelewa mzuri juu ya hatari zitokanazo na
malaria na hivyo kuwawezesha kuchukua tahadhali mapema.
2. Ushirikiano na Mashirika ya Kikanda ndani ya Afrika
Kwa kufanya
kazi na mashirika ya kikanda ili kushirikiana na Wakuu wa Nchi na Serikali
katika kujadili na kutatua changamoto kubwa na kutafuta majibu ya namna ya
kutokomeza kabisa ugonjwa wa malaria. Hii itajumuisha matumizi ya teknolojia
ili kuanzisha utaratibu wa kujitathimini na kufanya rejea kwa Wakuu wa Nchi na
Serikali, kubadilishana uzoefu na kushauriana namna bora zaidi za kufuata, na
kuanzisha tuzo kuwatambua wanaofanya vizuri zaidi katika ngazi ya kanda.
3. Mabaraza na Mifuko ya kutokomeza Malaria
Kuanzisha
walau Mabaraza mapya 15 ya kutokomeza
malaria na kutafuta fedha zitakazosaidia kuongeza zaidi ushirikiano wa
ngazi za juu wa sekta tofautitofauti ili kutia chachu juhudi za kupata fedha
zaidi za ndani ikiwemo kutoka katika sekta binafsi.
4. Makundi ya Ushauri ya Vijana
Kwa
kushirikiana na viongozi vijana toka maeneo mbalimbali ya kiuongozi barani
Afrika, kujenga “Jeshi la Vijana” dhidi ya malaria. Kikosi-kazi hiki cha mabalozi
vijana kitaanzisha ushirikiano wa kisiasa, utafutaji wa fedha, ubunifu, utafiti
na maendeleo na hata kuundwa kwa kada ya watu wanaopambana dhidi ya malaria.
“Vipaumbele
vya Mheshimiwa Rais Kenyatta tayari vimepata uungwaji mkono wa Umoja wa Afrika.
Tunatambua kwamba kufanikiwa kwa vipaumbele hivi vinne kutachochea zaidi
mapambano ya kuhakikisha Bara letu la Afrika linatokomeza kabisa ugonjwa huu,”
alisema Kamishina wa Masuala ya Jamii wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika,
Mheshimiwa Amira El-Fadil.
Dr. Abdourahmane
Diallo, ambaye ni Mtendaji Mkuu wa ushirikiano wa RBM wa Kutokomeza Malaria,
alisema, “Uongozi toka kwa viongozi wa nchi na serikali Barani Afrika ambao
kutokomeza malaria ni moja ya sera zao muhimu za kisiasa, ni muhimu sana katika
vita hii. Ninaamini kwamba vipaumbele vinne vya Rais Kenyatta, vikiongozwa na
ubunifu na ushirikishwaji wa wadau wote ndio njia sahihi ya kufikia malengo ya
kutokomeza malaria. Vitahakikisha pia kwamba kuna raslimali mpya na jamii mpya
zimejumuishwa kwenye vuguvugu hili la kutokomeza kabisa malaria.”
Ugonjwa wa
malaria unabaki kuwa changamoto kubwa inayolikabili bara la Afrika. Kiasi cha
93% ya wagonjwa wote wa malaria duniani wanapatikana Afrika huku 94% ya vifo
vyote ulimwenguni vinavyotokana na malaria navyo vikitajwa kutokea barani humo.
Kuna haja ya kuchukua hatua za haraka hasa katika mataifa 10 yaliyoko ndani ya
Umoja wa Afrika ambayo yanachangia 67% ya wagonjwa na 62% ya vifo ulimwenguni
kote. Mataifa hayo ni Nigeria, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda, Cote
d’Ivoire, Msumbiji, Niger, Burkina Faso, Mali, Angola na Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...