Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akifungua jana kongamano la siku mbili la vijana katika fursa za kilimo , mifugo  na uvuvi ambao wameoka  Tabora, Kigoma na Singida .

Vijana kutoka Tabora , Singida na Kigoma wakiwa katika kongamano  la siku mbili linalohusu fursa za kilimo , mifugo  na uvuvi. Kongamano hilo limefanyika jana mjini Tabora
 
NA TIGANYA VINCENT

VIJANA wametakiwa kutumia fursa zinazotokana shughuli za kilimo na ufugaji kujiari wenyewe badala ya kusubiri ajira za Serikali ili wawaze kujiongezea kipato kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akifungua kongamano la vijana katika fursa za kilimo , mifugo  na uvuvi kwa washiriki toka Tabora, Kigoma na Singida.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Nishati, imejitahidi kufikisha umeme vijijini ambako ndiko mazao yanapatikana ili kuweza kuyaongezea thamani kwa kuyasindika.

Mwanri alisema hiyo ni fursa nzuri kwa vijana ya kutumia umeme ilikufanya kazi za kuzalisha na kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi hivyo kuongeza thamani na uhakika wa soko na bei nzuri.Alisema uzalishaji wa mbegu bora za mazao nchini una uhitaji mkubwa na takwmi zinaonyesha kuwa mahitaji ya mbegu ni tani 187,000 kwa mwaka wakati uzalishaji wa ndani ni tani 71,000.

Mwanri aliongeza kuwa eneo hilo lina fursa kubwa kwa vijana kuzalisha mbegu kwani zinzhitajika kwa wingi.Alisema eneo jingine ambalo ni fursa kwa vijana ni kilimo cha mazao ya mafuta ambapo mahitaji ya mafuta ya kula ni lita 650,000 kwa mwaka wakati uwezo wa nchi ni kuzalisha lita chini ya 250,000.

Mwanri alisema hali hiyo inatoa fursa kubwa kwa vijana kuzalisha mazao ya alizeti na michikichi.

Kwa upande wa Mratibu wa Mkakati wa Taifa wa Vijana kushiriki katika Kilimo Revelian Ngaiza alisema lengo kongamano hilo ni kutoa elimu kwa vijana nchini ili waweze kushiriki katika uzalishaji mali kupitia kilimo na ufugaji ili waweze kuinua kipato cha na Taifa kwa ujumla.

Alisema kauli mbiu yetu ni “vijana,kilimo ni ajira” imelenga kuwasaidia vijana kutambua na kufanya kilimo kuwa nguzo ya upatikanaji ajira nyingi zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...