Na Karama Kenyunko
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema wako mbioni kuhuwisha sera ya teknolojia ili kuwezesha usimamizi wa kazi za ubunifu na kuongeza udhibiti kwenye kazi hizo.
Akizindua wiki ya ubunifu iliyoandaliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Watu (HDIF), Ole Nasha amesema serikali ya awamu ya tano inaangalia kwa ukaribu teknolojia na mawazo yenye tija yanayobuniwa kwa lengo la kufanikisha lengo la kuwa uchumi wa viwanda.
Alisema Tanzania ya viwanda haiwezi kufanikiwa kama hakuna wabunifu, ndiyo maana wako makini ili kuhakikisha wanapata mawazo mapya na yenye tija.
“Nafarijika kuona vijana wa Kitanzania wanaumiza vichwa kubuni mawazo na teknolojia ambazo zina manufaa makubwa katika kutatua changamoto katika jamii hivyo, vijana hasa wa maeneo ya vijijini sehemu ya utatuzi wa changamoto zilizopo kwenye jamii kubuni teknolojia," amesema Ole Nasha.
Ameeleza kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kuhakikisha bunifu zenye tija zinatumika kibiashara na kuleta manufaa kwa wabunifu.
Naye, Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa ubunifu wa maendeleo ya binadamu (HDIF) Joseph Manirakiza amesema ni wakati sasa kwa wabunifu kuanza kufikiria utatuzi wa changamoto zilizopo katika jamii.
“Tunaposema buni kwa tija ina maana yanahitajika yale mawazo yanayotatua changamoto tulizonazo. Kama hatuna wabunifu basi tutaendelea kubaki kama tulivyo,”
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema wako mbioni kuhuwisha sera ya teknolojia ili kuwezesha usimamizi wa kazi za ubunifu na kuongeza udhibiti kwenye kazi hizo.
Akizindua wiki ya ubunifu iliyoandaliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Watu (HDIF), Ole Nasha amesema serikali ya awamu ya tano inaangalia kwa ukaribu teknolojia na mawazo yenye tija yanayobuniwa kwa lengo la kufanikisha lengo la kuwa uchumi wa viwanda.
Alisema Tanzania ya viwanda haiwezi kufanikiwa kama hakuna wabunifu, ndiyo maana wako makini ili kuhakikisha wanapata mawazo mapya na yenye tija.
“Nafarijika kuona vijana wa Kitanzania wanaumiza vichwa kubuni mawazo na teknolojia ambazo zina manufaa makubwa katika kutatua changamoto katika jamii hivyo, vijana hasa wa maeneo ya vijijini sehemu ya utatuzi wa changamoto zilizopo kwenye jamii kubuni teknolojia," amesema Ole Nasha.
Ameeleza kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kuhakikisha bunifu zenye tija zinatumika kibiashara na kuleta manufaa kwa wabunifu.
Naye, Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa ubunifu wa maendeleo ya binadamu (HDIF) Joseph Manirakiza amesema ni wakati sasa kwa wabunifu kuanza kufikiria utatuzi wa changamoto zilizopo katika jamii.
“Tunaposema buni kwa tija ina maana yanahitajika yale mawazo yanayotatua changamoto tulizonazo. Kama hatuna wabunifu basi tutaendelea kubaki kama tulivyo,”
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha akizungumza na wadau wa maendeleo na wabunifu wakati akizindua Wiki ya Ubunifu 2020 leo jijini Dar es Salaam ambayo inakutanisha zaidi ya wadau na wabunifu 6,000
Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk Amos Nungu akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Ubunifu 2020 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...