Mkoa wa Pwani, WILAYA ya Mkuranga yasaji jumla ya Wabunge WALIOTIA Nia 15 na madiwani 190




Janeth Raphael, Michuzi Tv.








Na Janeth Raphael, Michuzi TV

JUMLA Ya watia nia wa kuomba ridhaa ya kuchaguliwa katika nafasi za ubunge 15 na udiwani 190 wamerudisha  fomu za kuwania nafasi hizo katika Mkoa wa Pwani Wilayani Mkuranga, ikiwa  ni sehemu ya mchakato unaoendelea nchi nzima kwa sasa kwa  hatua ya awali  ya kusaka wawakilishi wabunge na Madiwani.

Akizungumza na Michuzi Tv leo Wilayani humo Katibu wa CCM Wilaya ya Mkuranga Rukia Mbasha amesema kuwa Wilaya ya Mkuranga ina kata 25 na zoezi limekamilika salama na waliotia nia ya kugombea nafasi za Ubunge wamefikia 15 na nafasi za udiwani 190.

Aidha Katibu huyo Amesema kuwa;

 "kwa ujumla zoezi la uchukuaji fomu na kurudisha lilienda vizuri hapakuwa na changamoto yeyote na kumekuwa na mwamko mkubwa sana ukilinganisha na mwaka 2015." ameeleza.

Pia Mbasha amewapongeza wote waliojitokeza na amewaombea kwa Mungu kwa kila aliye sahihi Mungu ampe nafasi ya kuongoza wananchi na kutatua changamoto zao kwa weledi na kusukuma maendeleo ya nchi mbele katika kumsaidia Rais Magufuli na kusimamia ilani za chama hicho.

Mwisho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...