NA DENIS MLOWE,IRINGA
MADIWANI wa halmashauri ya Manispaa Iringa wamemwomba radhi mjumbe wa
halmashauri kuu ya CCM Taifa (Mnec) Salim Abri kutokana na maneno
mbalimbali aliyokuwa akitupiwa na baadhi ya wanachama na madiwani wa
manispaa.
Akizungumza kwa niaba ya madiwani wote wakati wakufunga mafunzo kwa
madiwani wa manispaa ya Iringa, Meya wa manispaa ya Iringa, Ibrahim
Ngwada alisema kuwa kitendo cha kuomba radhi kinatokana na maneno
mbalimbali ambayo amekuwa akitupiwa Mnec Salim Abri yaliyosababishwa na
madiwani wenyewe katika kipindi cha mchakato wa kumtafuta Meya na Naibu
meya wa Iringa.
Ngwada alisema kuwa kama kutupiwa matusi na maneno machafu
yamesababishwa na madiwani wenyewe kwenye jimbo la Iringa mjini kutokana
na homa ya uchaguzi wa nafasi hizo za umeya na unaibu meya hali ambayo
imewalazimu kumwomba radhi mnec.
“ Tunaomba tuchukue nafasi hii kukuomba sana radhi kwani sisi kama
madiwani wenzangu wamenituma nisimame mbele yao na mbele ya viongozi wa
chama kukuomba sana radhi na kama umetukanwa sana kwenye jimbo letu,
umedhalilishwa kwa namna yoyote na kama umeumia na familia yako imeumia
katika kipindi hichi cha uchaguzi ni sisi madiwani” alisema na kuongeza
kuwa
“ tumekutukana sisi wenyewe madiwani, tumewatuma watu wakutukane na
kukukashfu na hivyo hatuna sababu zilizopelekea kufanya vile lakini
tunasema tusamehe sisi”
Aliongeza kuwa wameomba radhi kwa kuwa wamemjeruhi yeye kama yeye na
familia yake, biashara anazofanya hivyo kutokana na kitendo hicho
madiwani wote wameomba radhi na kilichobaki ni kuungana na kushirikiana
katika kuwaletea maendeleo wanamanispaa ya Iringa.
Aidha walimwomba Mnec Salim kuwaombea radhi kwa viongozi wa CCM wilaya
na Mkoa kwa kuhusisha maneno machafu kwenye mchakato wa uchaguzi wa Meya
na Naibu Meya kitu ambacho hawakustahili kuhusishwa.
Ngwada aliongeza kuwa pamoja na mambo mbalimbali yaliyojitokeza kwa
kiwango kikubwa kipindi cha mchakato wa uchaguzi wa Meya na Naibu Meya
wametambua makosa , wamejutia makosa na kwa pamoja wameamua kushikamana
na kuondoa tofauti zote zilizojitokeza.
Alisema kuwa wameamua kuwa wamoja katika kusaidiana kuleta maendeleo ya
kata zote na endapo diwani yoyote ataleta mtengano na maneno ya
kuwavuruga na kugawa kwa pamoja vilevile watamgeukia na kuwa kinyume na
yeye na kuanzia sasa zitasikika pilikapilika za maendeleo.
Aidha Meya Ngwada alitumia nafasi hiyo kumshukuru na kumpongeza mnec
Salim Abri kwa kuwa na moyo wa kujitolea katika kusaidia na kufanikisha
ushindi wa kishindo wa CCM Nyanda za Juu Kusini kutoka na majukumu
aliyopewa kipindi cha uchaguzi na chama.
Kwa upande wake Mnec Salim Abri alipokea radhi hiyo kwa mikono miwili na
kuwataka madiwani kuijenga Manispaa na Kuwaletea Wananchi Maendeleo
waliyokuwa wakisubiri kwa kipindi kirefu.
Alisema kuwa wakati anakuja kufunga mafunzo hayo alikuwa anawaza vya
kuzungumza kuhusu madiwani lakini kutokana na maneno yaliyotolewa na
madiwani wote ya kuomba radhi hakika kwa mwanasiasa mkongwe hayo sio
majeraha hivyo amesamehe kwa moyo mkunjufu.
Alisema kuwa kuna wakati zikipita wiki moja au mbili hajatupiwa maneno
huwa anapata wasiwasi au amepoa lakini akianza kusemwa tu hapo mambo
yanakuwa barabara kabisa kwani kwenye siasa ukiwa husemwi wala
kuzungumzwa lazima hujitafakari kwani kuna kusemwa kwa ubaya au uzuri.
“Kuna msemo mmoja ulikuwa unatembea sana kwenye mitandao ya kijamii kama
wewe ni kiongozi na unataka kila mtu akupende acha siasa kauze ice
cream hivyo mimi siwezi kuacha siasa nikauze yoghurt wakati nimechagua
siasa.” Alisema
Alitumia nafasi hiyo kuwapongeza madiwani wote waliochagulia na
kuwahakikishia kuwapa ushirikiano wa kutosha katika kuwapa misaada
mbalimbali katika kata zao kwa kila mmoja pale ambapo watahitaji.
Aidha alisema kuwa changamoto mbalimbali zikiwemo ukosefu wa madawati,
madarasa atahakikisha wanayamaliza kwani imekuwa kil mwaka yanajitokeza
hali ambayo inemuumiza sana akili hivyo kwa kuwa manispaa iko chini ya
CCM watahakikisha wanamaliza changamoto hiyo.
.Mnec Salim Abri akizungumza na madiwani wakati akifunga mafunzo kwa ajili ya madiwani wa halmashauri ya Manispaa Iringa
Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada akizungumza
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...