Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Mark Ocitti (kulia) akimkabidhi zawadi ya kinywaji cha Johnnie Walker Mkuu wa Majeshi ya Ulinzia na Usalama mstaafu Generali George Waitara ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika mchezo wa Gofu. Hafla hiyo ilifanbyika jijini Dar es Salaam jana wakati wa kuhitimisha mashindano ya Johnnie Walker Waitara Trophy 2020.

Veterani wa mchezo wa Gofu Dkt. Edmund Mndolwa (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi 1,500,000/-mshindi wa kwanza ambaye ni mchezaji wa kulipwa (profesional player)  kutoka Klabu ya Gofu ya Lugalo Bryson Nyenza baada ya kuibuka mshindi katika mashindano ya Johnnie Walker Waitara Trophy yaliyodhamini na Kampuni ya Bia ya Serengeti Kupitia kinywaji chake cha Johnnie Walker.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Mark Ocitti (kulia) na Mkuu wa Majesi wa Malawi Generali Vincent Nundwe wakiingia uwanjani tayari kwa ajili ya kushiriki katika mashindano ya Walker Waitara Trophy 2020. Mashindano hayo ya siku moja yalifanyika jijini Dar es Salaam jana na yalidhaminiwa na Kumpuni ya Serengeti Breweries kupitia kinywaji cha Johnnie Walker.

Baadhi ya washiriki mashindano wa Johnnie Walker Waitara Trophy 2020, wakijiandaa kwa ajili ya mashindano hayo makubwa yaliyofanyika katika viwanja vya Gofu vya kijeshi vilivyopo Lugalo jijini Dar es Salaam na kushirikisha zaidi ya wachezaji 180 kutoka nje na ndani ya nchi.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...