Rais wa Marekani Donald Trump amesaini amri ya rais ya kupiga marufuku kampuni nane za China zenye program ya kutoa huduma ya ulipiaji wa bidhaa kwa njia ya mtandao.
Programu hizo ni pamoja na ile maarufu ya mtandao wa Alipay inayomilikuwa na mfanyabiashara tajiri China Jack Ma, QQ Wallet na WeChat pay.
Amri hiyo inaanza kutekelezwa ndani ya siku 45 baada yar ais kusema kuwa programu hizo zinapigwa marufuku kwasababu ni tishio kwa usalama wa taifa la Marekani.
Inasemekana kuwa kuna uwezekano program hizo zinatumika kufuatilia na kupata data za raia wa Marekani.
Programu zingine zilizopigwa marufuku ni pamoja na Tencent QQ, CamScanner, SHAREit, VMate na WPS Office.
"Marekani lazima ichukue hatua madhubuti dhidi ya waliotengeneza na kudhibiti programu za China kulinda usalama wa taifa letu," Amri hiyo ya rais imesema.
Aidha, amri hiyo ya Rais Trump inasema "kwa kufikia bidhaa za elektroniki za simu aina ya smartphones, tablets, na kompyuta, programu za China zinaweza kufikia taarifa muhimu za watumiaji ikiwemo taarifa nyeti za utambulisho na taarifa za kibinafsi."
Utawala wa Trump umeongeza shinikizo kwa makampuni ya China mwezi wake wa mwisho madarakani ikiwemo kampuni anazozichukulia kuwa zenye kuhatarisha usalama wa taifa hilo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...