Na Mwandishi wetu,
TAASISI
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini TAKUKURU Mkoani Manyara imetoa
onyo kwa wafanyabiashara wa madini ya tanzanite wa Mji mdog wa Mirerani
Wilayani Simanjiro wanaoendelea kutorosha madini hayo bila kulipa tozo
za Serikali.
Mkuu
wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara Holle Joseph Makungu, ametoa onyo hilo
alipokuwa akitoa taarifa ya taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu
iliyopita kwa waandishi wa habari Mjini Babati.
Makungu
amesema kuwa kuna baadhi ya wafanyabishara wanaendelea kutorosha madini
hayo kwa kukwepa kulipa tozo za serikali, kitendo ambacho ni kinyume
cha kanuni za madini za mwaka 2019.
Hata
hivyo, amesema Mkuu wa TAKUKURU wa kituo maalumu cha Mirerani Sultan
Ngaladzi na Ofisa madini mkazi wa Mkoa wa kimadini wa Mirerani, Fabian
Mshai wamekuwa wakitoa elimu kwa wadau wa madini ya hayo Tanzanite.
Amesema
katika semina hizo wamewatahadharisha juu ya ukiukwaji wa usafirishaji
wa madini ambapo taarifa za kiintelejensia zinaonyesha kuwa
walijitokeza wafanyabiashara wa nje wasio waaminifu ambao wamekuwa
wakichepusha madini ya Tanzanite na kuyapeleka masoko ya nje ya nchi
badala ya kuyapeleka kwenye masoko ya ndani yaliyofunguliwa na Serikali
kwa shughuli hiyo.
"Kwa
mujibu wa kanuni ya 12 ya usafirishaji wa madini ya mwaka 2019
wafanyabiashara wanapaswa kufanyiwa tathimini ya madini yao na kulipia
mrahaba, tozo ya ukaguzi na tozo ya huduma katika kituo maalumu cha
ukaguzi kikichopo jengo la one stop centre Mirerani, " amesema Makungu.
Aidha
mkuu huyo wa TAKUKURU Manyara amezitaka tasisi zinazodaiwa na Wakala wa
Ufundi na Umeme TAMESA mkoani Manyara kulipa madeni yao haraka kabla
hawajachukuliwa hatua za kisheria.
Amesema
katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita TAKUKURU Manyara imefanikiwa
kuwarejeshea fedha na mali mbalimbali baadhi ya watu waliokuwa
wamekopeshwa mikopo isiyo na lesenimikopo umiza, imetoa elimu ya rushwa
mashule na imedhibiti miradi 11 ya zaidi ya shilingi bilioni 1
iliyokuwa kwenye mazingira ya kuhujumiwa.
Pia
Taasisi hiyo ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Manyara, imeanzisha ofisi
inayotembea maarufu PCCB mobile ambayo inawafuata wananachi maeneo yao
na kusikiliza kero zao.
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Hole Joseph Makungu akizungumza na waandishi wa habari Mjini Babati
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...