Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
TATU
Bakari Hassan ,mkulima mwenye miaka 55 ,amejeruhiwa mguu wake wa kulia
kwa kupigwa risasi akiwa shambani kwake ,baada ya kudhaniwa kuwa yeye ni
nyani.
Jeshi la polisi mkoani Pwani ,linamshikilia mkulima Mhina Mrisho Ally (47)anaedaiwa kumjeruhi mkulima huyo.
Kamanda
wa polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa ,ameeleza,pia mtuhumiwa Mrisho
alipokwenda kupekuliwa nyumbani kwake alikutwa na bunduki mbili aina ya
gobore ambazo anazimiliki kinyume na sheria.
Wakati huo huo,
jeshi hilo linawashikilia wahamiaji haramu sita ,raia wa Malawi,
waliokuwa wakisafirishwa kutoka Mbeya kwenda Dar es salaam,kinyume na
sheria huku wakiwa wameingia nchini bila vibali.
Wahamiaji
hao haramu wamekamatwa eneo la Tanita, Kibaha pamoja na dereva wa gari
namba T.703 DTR aina ya Toyota hiace jina limehifadhiwa mkazi wa Uyole
Mbeya.
Wankyo alieleza, wahamiaji hao walikuwa wanapelekwa Dar es salaam kufanya kazi ya kuuza bar na kusuka..
Alitoa
siku saba kwa wale wote wanaomiliki silaha bila vibali kuzisalimisha
silaha hizo na wakibainika katika operesheni za kipolisi basi hatua kali
zitachukuliwa.
Pia alikemea madereva wanaohusika kusafirisha wahamiaji haramu kuacha Mara moja na wakikamatwa dola itachukua mkondo wake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...