SERIKALI imesema itahakisha miradi ya maji inakamilika kwa wakati kwa kuwezesha upatikanaji
wa rasilimali fedha ili jamii iweze kunufaika na huduma ya maji safi na salama kupitia
mradi wa maji wa Mabokweni, katika Jiji la Tanga.
Kauli
hiyo imetolewa hii leo na Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso mara baada ya
kutembelea mradi wa Maji wa Mabokweni unaotekelezwa katika Jiji la Tanga kufuatia
ombi la Mbunge wa Tanga Mjini Mhe. Ummy Mwalimu ambae pia ni Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).
Mhe.
Ummy Mwalimu amesema mradi wa maji wa Mabokweni umekwama kwa muda mrefu na
kusababisha wakazi wa maeneo hayo na vitongoji vya Mzizima na Chongoleani
kukosa maji safi na salama.
“Mhe.
Waziri wa Maji, hapa Tanga mjini maji yanapatikana isipokuwa katika maeneo machache,
kukamilika kwa mradi huu kutawezesha kutatua kero ya maji ya muda mrefu kwa wananchi
wangu” Ummy Mwalimu alisisitiza.
Amesema
pia changamoto nyingine inayowakabili
wakazi wa Tanga mjini ni bili kubwa za maji ambapo baadhi yao wamesitishiwa
hudumu hiyo kutokana na kutozwa bili kubwa zisizolipika.
Kwa
upande wake Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso amesema azma ya Serikali ya Awamu ya
Tano ni kuhakikisha kuwa inaboresha upatikana wa huduma maji mijini na vijijini.
“Serikali
ina wajibu wa kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa wananchi wake
haiwezekani bili za maji kuwa kubwa kiasi hiki, naagiza badala ya kuuziwa ndoo
moja kwa shilingi mia moja, sasa iuzwe kwa Shilingi hamsini tu hapa Kibafuta”
Aweso alisisitiza.
Amemuagiza
Meneja wa RUWASA kuhakikisha fedha zitakazotolewa zinatumika kwa kazi
iliyokusudiwa ili mradi huo ukamilike ndani ya muda mfupi.
Katika
ziara ya siku moja ya kukagua miradi ya maji katika Jiji la Tanga, Waziri wa
Maji Jumaa Aweso na Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Mhe. Ummy Mwalimu wametembelea
Mradi wa Maji wa Mabokweni katika Kijiji cha Kiruku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...