Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
KITUO
Cha kupozea umeme kilichopo Mlandizi ,mkoani Pwani kinatarajia kuongeza
uwezo wa upatikanaji wa Umeme MVA 120 ,ifikapo mwezi march mwaka huu na
baadae itaongezeka na kufikia MVA 240 kwa mwaka 2022.
Lengo
kuu la kuongeza kasi katika upatikanaji wa nishati ya umeme imetokana
na mahitaji makubwa ya umeme viwandani na majumbani kutoka 60 mwaka 2015
na kufikia 117.8 mwaka huu.
Hayo
yamebainika wakati mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo
alipokwenda kutembelea kituo hicho ambacho kiliungua na kusababisha
changamoto ya upungufu wa umeme ambapo kimefanyiwa maboresho na kuongeza
transfoma itakayowashwa mwezi ujao na kuongeza upatikanaji wa umeme wa
MVA 120.
Ndikilo alisema,
ameridhishwa na kasi ya shirika la umeme Tanesco chini ya meneja
mhandisi Mahawa Mkaka ,kutekeleza kwa vitendo mpango mkakati unaoendana
na mahitaji ya umeme na hatimae kufikia adhma ya mkoa ya UKANDA wa
viwanda .
"Kituo hiki
kinapeleka pia umeme maeneo ya viwanda Zegereni kwenye viwanda 25 na
majumbani, Bandari kavu ya Kwala na kina hudumia wateja 182,000 kati ya
hao ni viwanda vya kati na vikubwa 322 ,hongereni sana 'alieleza Ndikilo
.
Aidha,aliitaka Tanesco
kushughulikia changamoto ya Mkuranga kuendelea kupata umeme kituo cha
umeme Mbagala wakati wilaya hiyo imesheheni kwa viwanda hivyo iondokane
na kutegemea umeme katika kituo hicho.
Hata
hivyo Ndikilo alielekeza taasisi nyingine wezeshi ya DAWASA na ile
inayohusika na barabara kuendana na kasi ya mkoa kuinua sekta ya
uwekezaji kwa kufikisha huduma muhimu maeneo ya viwanda .
Awali
akitoa taarifa ya utekelezaji na maboresho ,meneja wa Tanesco mkoani
Pwani ,mhandisi Mahawa Mkaka alisema,mwaka 2018-2020 walikuwa
wakihudumia viwanda 1,275.
"
Tunaishukuru serikali ya awamu ya tano kwani tumeweza kuwa na miradi
mingi ikiwemo mradi wa REA III awamu ya kwanza uliogharimu bilioni 37 na
kufikia wateja zaidi ya 6,000,mradi wa Peri-Urban bilioni 65 na
kuunganisha maeneo 178 na mradi wa ujazilizi ambao unatarajia kuanza
bilioni 10 ambapo maeneo 116 yatafikiwa"alifafanua Mkaka.
Mkaka
alieleza, miradi ya Tanesco kwa mwaka wa fedha 2021-2022 itagharimu
bilioni 10.2 kwa ajili ya kuboresha sekta hiyo na kusogeza huduma ya
umeme maeneo 121.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...