Na Mwandishi wetu

Dar es Salaam. Jumla ya klabu tisa (9) za mchezo wa kuogelea zimethibitisha kushiriki katika mashindano ya Taliss yaliyopangwa kufanyika kwenye bwawa la kuogelea la klabu ya Gymkhana jijini Dar es Salaam.

Meneja wa klabu ya Taliss, Hadija Shebe amezitaja klabu hizo kuwa ni  Dar es Salaam Swimming Club (DSC), Bluefins, Mis Piranhas, Champion Rise, UWC Moshi, Wahoo (Zanzibar)  na wenyeji, Taliss. Pia zipo klabu za  Bluefins, Mwanza Swimming Club na  FK Blue Marlins.

Hadija alisema kuwa wanatarajia kuwa na mashindano yenye ushindani mkubwa kutokana na ukweli kuwa mashindano hayo ni ya kwanza tokea kuruhusiwa kwa michezo nchini Juni Mosi mwakani/ 

Alisema kuwa pamoja na serikali kuruhusu kuendelea kwa michezo, bado mchezo wa kuogelea ulishindwa kufanya shindano hapa moja kwa mujibu wa kalenda ya chama cha mchezo huo nchini kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao.

“Waogeleaji walikuwa wanafanya mazoezi tu. Haya ndiyo mashindano ya kwanza kwa mujibu wa kalenda ya michezo ya TSA na hivyo tunatarajia ushindani mkubwa kutoka kwa waogeleaji ambao wamejifua kwa muda mrefu sana,” alisema Hadija.

Hadija alisema kuwa ili kuleta ushindani katika mashindano hayo, kila muogeleaji atatakiwa kuchagua kushindana kwenye aina sita ya mashindano na matukio mawili kwa ajili ya relay.

“Hivyo kila muogeleaji atashindana katika vipengele nane katika staili tano za kuogelea ambazo ni backstrokes, butterflies, individual medleys, breaststrokes na freestyles. Tunawaomba wadhamini kusaidia mashindano haya ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya mchezo huo nchini. Mwisho wa kuthibitisha kushiriki ni Jumamosi (Februari 13), kwa sasa tunawaomba viongozi wa klabu nyingine ambazo hazijathibitisha kufanya   kwa mujibu wa taratibu,” alisema.
 
Olivia Swart akishindana katika mashindano yaliyopita.

. Nathan Kagoro wa klabu ya Taliss akichapa maji wakati wa mashindano yaliyopita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...