Na Woinde Shizza , Michuzi Tv-Arusha
Shirika
la Umeme Tanesco limejipanga kuhakikisha umeme unafika maeneo yote
ambayo wananchi wanahitaji kwa lengo la kuendeleza uchumi wa wananchi
,mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla .
Hayo
yamebainishwa na kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoa wa
Arusha Mnhandisi Andrew Lucas Ako wakati akiongea na waandishi wa
habari kwenye maonyesho ya nne ya mifuko ya programu uwezeshaji wananchi
kiuchumi yanayofanyika mkoani hapa Katika viwanja vya kumbukumbu ya
Sheikh Amri Abeid, ambapo alisema kuwa kwa upande Arusha jiji wameweza
kuunganisha umeme kwa wananchi kwa asilimia 80 , na asilimia 20
iliobaki wanapambana kumalizia na wanaamini Katika awamu hii ya miaka
mitano watamalizia asilimia zilizobaki.
Alibainisha
kuwa katika jitihada za kuisaidia serikali kuwezesha wananchi kiuchumi
shirika la Umeme Tanesco linahakikisha maeneo yote ambayo wananchi
wanahitaji umeme ,yanawekwa kwa bei nafuu na maeneo mengine wananchi
wanawekewa umeme kwa gharama za Shirika kutokana na uhitaji wa wananchi
lengo kubwa ni kuhakikisha wanapata mahitaji yao ya msingi.
Alisema
kuwa shirika la umeme Tanesco lipo Katika maonesho hayo kwa ajili ya
kutoa elimu kwa wananchi wote wanaofika katika maonesho hayo kuhusu huduma
zinazotolewa na shirika hilo ,pia wajue miradi mbalimbali ambayo
inatekelezwa na tanesco mkoa wa Arusha .
"Sasa
hivi tuna miradi mikubwa na midogo ambayo tunatekeleza kama mkoa kwa
bajeti ya mwaka 2020/2021 ,miradi midogo tunayotekeleza ina gharimu
kihasi cha shilingi bilioni 10 kwa Arusha na hadi sasa tumeshatekeleza
kwa asilimia 80 na tunaamini adi ifike mwezi wa nne tutakuwa
tumekamilisha "alibainisha Ako.
Akifungua
maonyesho hayo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alivitaka vyombo mbalimbali
vya habari kushiriki kikamilifu katika maonesho hayo ili viweze
kufikisha ujumbe sahihi kuhusu fursa za uwezeshaji wananchi kiuchumi
kupitia mifuko na programu za uwezeshaji kwa wananchi wote nchini.
Alibainisha
kuwa tathmini za mara kwa mara zinazofanywa na Serikali kuhusu
utendaji wa Mifuko na Program za Serikali za uwezeshaji zinaonesha
kwamba mifuko hiyo na programu hizo zimechangia kwa kiwango kikubwa
jitihada zake za kukuza uchumi na kupunguza umaskini..
wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanesco wakiwa katika banda lao lililopo Katika maonyesho ya nne ya mifuko programu uwezeshaji wananchi kiuchumi yanayofanyika Katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid mkoani ArushaKaimu Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoa wa Arusha Mhandisi Andrew Lucas Ako akiongea na waandishi wa habari Katika maonyesho hayo
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mrisho Gambo wa kwanza kushoto akibadilishana mawazo na baadhi ya waandishi wa habari waliouhudhuria maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi
wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanesco wakiwa katika banda lao lililopo Katika maonyesho ya nne ya mifuko programu uwezeshaji wananchi kiuchumi yanayofanyika Katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid mkoani ArushaKaimu Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoa wa Arusha Mhandisi Andrew Lucas Ako akiongea na waandishi wa habari Katika maonyesho hayo
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Mrisho Gambo wa kwanza kushoto akibadilishana mawazo na baadhi ya waandishi wa habari waliouhudhuria maonesho ya nne ya mifuko ya programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...