HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imezindua kitabu cha muuguzi cha utambuzi wa tatizo kwa mgonjwa (Nursing Diagnoses for Academic and clinical Practice) ambacho kitainua ubora wa huduma za kiuuguzi na ukunga.

Kitabu hicho kimeandikwa na Afisa Muuguzi wa Muhimbili-Mloganzila Bw.Wilson Fungameza ambapo pamoja na mambo mengine kinalenga kuongeza umahiri wa utendaji kazi na kusaidia kudumisha huduma za kiuguzi kulingana na hali ya mgonjwa kwani kimefuata mfumo uliothibitishwa na viwango vya utoaji wa huduma za kiuguzi na ukunga Duniani.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga & Mloganzila Dkt. Thecla Kohi amesema kitabu hicho ni hazina kubwa kwakua kinaweza kutumiwa na walimu na wanafunzi katika taaluma ya uuguzi na ukunga.

Dkt. Kohi ambaye alikua mgeni rasmi katika uzinduzi wa kitabu hicho amewasihi wataalamu wa afya kuendelea kuwa wabunifu na kuandika machapisho mbalimbali ili kuleta mabadiliko katika utoaji wa huduma.

“Ninatambua mchango mkubwa wa uongozi wa Muhimbili-Mloganzila kwa kuwezesha kufanikisha jambo hili muhimu , napenda kutumia fursa hii kutoa rai kwa taasisi za afya kuendelea kushirikiana na watumishi ili kutambua na kukuza vipaji vyao”amesema Dkt. Kohi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Lawrence Museru amesema endapo kitabu hiki kitatumika vizuri kitaongeza tija katika utendaji kazi na kuleta matokeo chanya ya utoaji wa huduma za afya.

“Endapo tukisoma vizuri na kutumia ujuzi uliomo humu ni matumaini yangu kuwa utendaji wa wauguzi na wakunga utaendelea kukua na huduma kuwa bora zaidi” amesema Prof.Museru.

Aidha Prof. Museru amewataka watalamu wa afya kutosubiri kuandikiwa vitabu na wataalamu wengine kutoka nje ya nchi bali watumie ujuzi wao kuandika vitabu ambavyo vitaendana na mazingira halisi.

Kwa upande wake mwandishi wa kitabu Bw.Wilson Fungameza ameiomba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na wadau wengine kuingiza kitabu hicho kwenye mitaala ya kufundishia vyuoni na maeneo ya kazi ili wataalamu wengi wa afya waweze kukitumia.


Mjumbe ya Bodi ya Wadhamini ya MNH Dkt. Tecla Kohi (wapili kutoka kulia) akikata utepe ikiwa ishara ya uzinduzi wa kitabu, katikati ni Mkurugenzi Mtendaji Prof. Lawrence Museru, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Muhimbili-Upanga Sis. Zuhura Mawona, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Msaidi wa Huduma za Uuguzi Muhimbili-Mloganzila Sis. Redemptha Matindi.
Baadhi ya watumishi wakimsikiliza mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa kitabu cha muuguzi cha utambuzi wa tatizo kwa mgonjwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...