Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi akiteta jambo na mwanamuziki galacha duniani katika muziki wa rhumba, Koffi Olomide aka Mzee ya Mboka, walipokutana usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam ambapo mwanamuziki huyo alikuwa nchini kutumbuiza chini ya mwaliko wa kampuni ya Prime Time Promotions na Clouds Intertainment.

Dkt. Abbasi alitumia muda huo kumshukuru mkongwe huyo kwa kuitangaza Tanzania mara kwa mara ikiwemo kushirikiana na wanamuziki vijana wa hapa nchini kuinua na kuutangaza muziki wao. Koffi aliahidi kuendelea kusaidia kukuza vipaji vya Tanzania akisema: "Dar es Salaam na Tanzania mimi ni kama nyumbani, nitaendelea kuwa nanyi karibu."

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi akiwa katika picha mbalimbali na Mwanamuziki Koffi Olomide kutoka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyekuwa akitumbuiza katika tamasha la Mahaba ya Rhumba Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi  akimsikiliza  Mwanamuziki Koffi Olomide kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyekuwa akitumbuiza katika tamasha la Mahaba ya Rhumba Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi  akimueleza jambo  Mwanamuziki Koffi Olomide kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyekuwa akitumbuiza katika tamasha la Mahaba ya Rhumba Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...