Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb) akiwa amesimama wakati wimbo wa Taifa wa Msumbiji ulipokuwa ukipigwa wakati wa ufunguzi wa kikao cha Utatu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-TROIKA) kilichofanyika kwa njia ya mtandao . Kikao hicho kilijumuisha nchi za Msumbiji Mwenyekiti, Tanzania Mwenyekiti aliyepita na  Malawi Mwenyekiti ajaye,


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb) akiandika kitu wakati wa kikao cha SADC-TROIKA) kilichofanyika kwa njia ya mtandao 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb) akizungumza katika kikao cha SADC-TROIKA) kilichofanyika kwa njia ya mtandao ambacho kiliridhia pendekezo la kuendesha vikao vya Jumuiya kwa mtandao 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (katika Screen) akishiriki kikao cha Maafisa Waandamizi wa SADC TROIKA ambacho pia kilifanyika kwa njia ya Mtandao. 

===  =====  ======
Kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Utatu wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC- TROIKA ) kilichofanyika kwa njia ya Mtandao kimeridhia mapendekezo ya Mawaziri wa Afya wa SADC kutaka kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC kifanyike kwa njia ya Mtandao ili kukabiliana na janga la ugonjwa wa COVID 19 katika ukanda wake.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb) aliyeshiriki kikao hicho cha SADC Troika akimuwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema kikao hicho kilikutana kwa ajili ya kupitia na kujadili mapendekezo ya Mawaziri wa afya wa SADC kilichofanyika Februari 29, 2021.

Amesema Mawaziri wa Afya walipendekeza kuwa kikao cha Baraza la Mawaziri kifanyike kwa njia ya mtandao na kikao cha Wakuu wa Nchi kilichokuwa kifanyike mwezi Machi kisogezwe mbele ambapo sasa kitafanyika kati ya mwezi Mei au Juni kutegemeana na hali ya maambukizi ya ugonjwa wa COVID 19 itakavyokuwa na kuongeza kuwa vikao vingine vyote vitafanyika kwa njia ya mtandao hadi hapo hali ya maambukizi itakapokuwa imetengemaa.

Vikao hivyo viwili vilikuwa vifanyike mwezi Machi ana kwa ana nchini Msumbiji

Utatu wa SADC-TROIKA kwa sasa unaundwa na nchi za Msumbiji, Tanzania na Malawi umefanya lichofanyika kwa njia ya mtandao kulikutana kujadili taarifa ya kikao cha Mawaziri wa Afya wa SADC kilichokaa tarehe 29 Februari kuangalia hali ya ugonjwa wa COVID 19 katika ukanda wa SADC ambacho kiliamua kuwa kikao cha Baraza la Mawaziri kifanyike kwa njia ya Mtandao

Kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha maafsa waandamizi ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge alishiriki kikao hicho ambacho pia kilifanyika kwa njia ya Mtandao.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...