Na Woinde Shizza ,Michuzi Tv

Mganga mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi amewataka wananchi kujenga tabia ya kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa ya kuambukiza pamoja na yale yasiyo ya kuambukizwa.

Aliyasema hayo leo  wakati akiongoza mazoezi ya pamoja akiwa na watumishi wenzake kutoka Wizara ya Afya ,ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa pamoja na wananchi wa jiji la Dodoma mazoezi yalifanyika katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma.

Alisema kuwa wananchi wengi wamekuwa na mazoea ya kukaa bila kufanya mazoezi jambo ambalo linawasababishia kushambuliwa na magonjwa mara kwa mara.

"Mazoezi yanasaidia sana  kuondoa magonjwa yasiyoambukiza kama sukari  na presha ,pia huondoa usongo wa mawazo pamoja na kuleta mahusiano baina ya kundi na kundi ,mtu na mtu au na jamii nzima na muunganiko wa kazi kupitia mazoezi hayo"alibainisha Makubi.

Aidha mbali na kufanya mazoezi mganga mkuu  wa Serikali pia alishiriki katika zoezi  la uhamasisha wananchi kufanya usafi kwa kushiriki zoezi la kufanya usafi wa mazingira katika uwanja wa Nyerere square.

 Akiongea  wakati wa kufanya usafi huo  amewataka wananchi kuimarisha usafi wa mazingira ili  kujikinga na magonjwa ya kuambukiza.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...