Na Munir Shemweta, WANMM
Serikali
imewaonya wamiliki wote wa ardhi wanaoharibu, kung'oa na kuhamisha
alama za upimaji ardhi (Beacons) na kueleza kwamba watakaobainika
watachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kulipa faini ya shilingi 750,
000 au kifungo cha mwaka mmoja jela.
Kwa
mujibu wa taarifa ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
kupitia kitengo chake cha Mawasiliano Serikalini ni kosa kisheria
kufanya shughuli yoyote inayoweza kusababisha kuharibu, kung'oa au
kuhamisha alama za upimaji.
Taarifa
hiyo imeeleza kuwa, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
imebaini uwepo baadhi ya wananchi wanaoharibu, kung'oa na kuhamisha
alama za upimaji na kubainisha kwamba, kitendo hicho ni kinyume cha
sheria.
Kupitia taarifa
yake Wizara ya Ardhi imeeleza kuwa, kutokana na kukithiri vitendo hivyo
inawakumbusha wananchi wote kuwa mtu yeyote atakayebainika kuharibu,
kung'oa, kuhamisha au kufanya shughuli inayoweza kuharibu alama za
upimaji ardhi atakuwa ametenda kosa la jinai na atawajibika kulipa faini
shilingi 750,000 au kifungo cha mwaka mmoja jela au adhabu zote kwa
pamoja.
Wizara ya Ardhi
imewaasa wananchi wote kutojihusisha na vitendo hivyo kwa kuwa
vinarudisha nyuma jitihada za serikali za kuongeza usalama wa miliki
ardhi kwa wananchi.
Wizara
ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imekuwa ikipanga, kupima na
kumilikisha ardhi kwa lengo la kuongeza usalama wa miliki za ardhi kwa
wananchi na maeneo yote yaliyopangwa na kupimwa yamewekewa alama za
upimaji ardhini ( Beacons) kwa mujibu wa sheria ya upimaji ardhi sura ya
324.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...