*Mhandisi wa Kanda ya Mashariki TCRA ataka matakwa ya leseni kuzingatiwa
Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekabidhi leseni ya Kituo cha Televisheni cha Hope kilicho chini ya Taasisi ya Vyombo vya Habari vya Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania.
Akizungumza na kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba, Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka hiyo Mhandisi Lawi Odiero amesema kuwa kituo hicho kifuate sheria na kanuni zilizopo katika leseni hiyo.
Amesema kuwa Mamlaka kama wadhibiti hawata acha kuchukua hatua pale panapotokea kukiukwa kwa leseni.Aidha amesema kuwa kupatikana kwa leseni ni jambo moja lakini jambo la kufuata nasharti ya leseni inavyotaka.
Amesema kuwa Mamlaka kama wadhibiti hawata acha kuchukua hatua pale panapotokea kukiukwa kwa leseni na kwamba kupatikana kwa leseni ni jambo moja lakini jambo la kufuata nasharti ya leseni inavyotaka ni muhimu zaidi .
Amesema kuwa Mamlaka kama wadhibiti hawata acha kuchukua hatua pale panapotokea kukiukwa kwa leseni.
Aidha amesema kuwa kupatikana kwa leseni ni jambo moja lakini jambo la kufuata nasharti ya leseni inavyotaka.
Kwa upande wake Mchungaji na Mkurugenzi wa Taasisi ya Vyombo vya Habari vya Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Christopher Ungani amesema kuwa mpaka wanafika hatua ya kupokea leseni wamepata msaada mkubwa kutoka TCRA.
Amesema kuwa watafuata masharti ya leseni na kanuni pamoja na miongozo katika kutoa huduma ya kuhabarisha wananchi kitaifa.
Ungani amesema mara nyingine wakifika TCRA waende kwa mambo ya kujenga na sio ya ukiukaji wa leseni waliyopewa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...