Taarifa za BBC, zinaeleza shuhuda amesema nusu ya wanafunzi waliotekwa hakuna mwanafunzi wa kiume kati ya waliotekwa.
Hayo yamethibitishwa na Kamishna wa ulinzi wa ndani na mambo ya ndani Ndg. Samuel Aruwan, ambae ameeleza kwamba ni kweli na uchunguzi unaendelea.
Msemaji wa Polisi, ASP Mohammed Jalige alisema idadi kamili ya wanafunzi hao wa kike waliotekwa bado haijajulikana.
Amesema Polisi wanafanya kazi kwa kushirikiana na Jeshi la Nigeria kuwafuatilia watekaji na kuhakikisha wanawaokoa wanafunzi hao.
Kamishna wa ulinzi wa ndani na mambo ya ndani, Ndg. Samuel Aruwan, alifanya mahojiano na channels za TV mbalimbali Nigeria, alipokuwa akitoa taarifa hizo.
Endelea kufuatilia ukurasa huu kwa taarifa mbalimbali za kisiasa, uchumi, biashara, burudani, michezo kijamii n.k.
#MichuziTV
#ChaguaKupambana
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...